ULAZIMA WA KUMSWALIA MTUME
MUHAMMAD (S.A.W.W) NA AALI ZAKE.
Sisi Mashia tunaamini kuwa kila
anapotajwa Mtume ni lazima tuitikie swalallahu alayhi wa aalihi wa salam (s.a.w.w).
Hii inatokana na agizo la Allah
pale ambapo yeye mwenyewe anatangaza wazi kuwa humtakia rehema Mtume, pale
aliposema;
“Hakika
Allah na Malaika wake wanamtakia Rehema Mtume. Enyi ambao mmeamini mtakieni
rehema juu yake na Msalimuni kwa (uzuri) wa Salamu.” (33:56).
Katika Aya nyingine ya Qur’ani
Tukufu, Allah anasema. “Amani na iwe juu ya watu wa Ya Sin (Ahl Ya Sin),” yenye
maana ya kizazi cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).
Aya hii inatuagiza kuwa
tunapomtakia rehema Mtume ni lazima tuwatakie rehema kizazi chake pia kwa
sababu yeye Allah ametuonyesha mfano ili nasi tuige kufanya hivyo.
Watu Wa Ya Sin Inawahusu Watu
(Ahlulbayt) Wa Muhammad (s.a.w.w).
Wafasiri wote na Wanachuo wa
madhehebu ya Ahlul Sunnah waljamaa wanakiri kwamba Allah amemuita Mtume kwa
jina Ya Sin. Hivyo basi Ahli (watu wa) Ya Sin maana yake ni watu wa Muhammad.
Miongoni mwa wengine, Ibn Hajar Makki, Mwanachuo wa Kisunni pamoja na kuwa na
chuki sana dhidi ya Shia, lakini anasema katika “Sawa’iq Muhriqa” chini ya aya
zilizonukuliwa katika kuwasifu Ahlul Bait, kwamba kikundi cha Wafasiri wamemnukuu
Ibn Abbas (Mfasiri mkubwa wa Waumini) akisema kwamba Ahl Yasin maana yake ni
Ahl Muhammad.
Kwa hiyo, Salaam, maamkuzi ya
amani kwa Ahli Ya Sin yana maana Salaam kwa Ahli Muhammad.
Imam Fakhru’d-Bin Razi
anaandika: “Ahli Bait wa Mtume wako sawa naye katika mambo matano:
1) Salaam: Salaam kwa Mtume na
Salaam kwa Ahli Ya Sin (Ahli Muhammad) ni kitu kimoja.
2) Salawat (kutakia rehma)
katika Swala kwa Mtume na Ahlul Bait wake, ambako ni lazima.
3) Tohara: Allah Anasema katika
sura ya “Ta Ha” (20:1): “(Ewe Mtume) Msafi na tohara:” Ile aya ya tohara
iliteremshwa katika kuwatukuza Ahlul-Bait (33:33).
4) Uharamu wa Sadaka: Sadaka
haiwezi kupokelewa imma na Mtume au Ahlul-Bait wake.
5) Mapenzi: Mapenzi kwa Mtume
maana yake ni mapenzi kwa Ahlul Bait wake.
Ndugu waislamu tujitahidi sana
kumtakia rehema Mtume na Ahlulbayt wake ili tuweze kufaidika na malengo
matukufu ya Allah kutokana na maagizo yake haya. Kinyume na hivyo ni balaa
kwetu. Hapa ninakusudia wale wanaochukia kusikia neno ahlulbayt na humtakia
rehema Mtume basi bila kuwataja Ahlulbayt wake kwa madai kuwa Uislamu hauna
uhusiano na ukoo wa Mtu. Watu hawa wamepata hasara kubwa maana wamepoteza faida
kubwa ya kuombewa msamaha na Ahlulbayt na swala zao hazikubaliwi.
Comments
Post a Comment