MTUME ALIANZA KWA KUUTANGAZA
UISLAMU KWA SIRI
Assalaam alaykum. Kwanza kabisa
nakupongezeni kwa kufunga mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Namwomba Allah atukubalie
dua, funga na amali zetu zote katika mwezi huu na katika miezi mingine pia.
Mara ya kwaza kabisa wakati
Mtukufu Mtume alipokuwa akiwalingania watu kuukubali ujumbe wa Uislamu,
alikumbana na upinzai wa kuhuzunisha na mkali sana. Kwa sababu ya umuhimu kwa
hiyo, alilazimika kutangaza ujumbe wake kuanzia hapo kwa siri kwa muda wa miaka
mitatu hadi yeye alipoagizwa tena na Allah (s.w.t.) kuwaita ndugu zake wa
karibu kabisa ili kuukubali ujumbe wake. Aliandaa karamu ya ndugu na akawaalika
takriban watu arobaini wa ukoo wake.
Katika mkusanyiko huo,
Muhammad (S.A.W.W) aliwauliza kama waliwahi kamwe kumuona akidanganya au kusema
uongo? Majibu ya jumla yakawa: “Hatujakuona wewe ukisema uwongo.” Kisha
akauliza: “Kama ingekuwa niwaambie kwamba maadui zenu wamejikusanya nyuma ya
vile vilima vya mchanga, tayari kwa kuwashambulia, je mngeniamini?” Wao
wakajibu, ‘Ndio.’
Halafu akasema: “Simjui mtu
yeyote katika Bara Arabu ambaye anaweza kuwapa ndugu zake kitu bora zaidi hasa
kuliko ninavyofanya sasa. Mimi ninakupeni furaha ya maisha yote; ya dunia hii
na yale ya kesho Akhera.
Mwenyezi Mungu ameniagiza
mimi kuwaiteni ninyi kwake. Ni nani kwa hiyo, miongoni mwenu atakayenisaidia
katika hili, ili awe ni ndugu yangu, mrithi wangu na khalifa wangu baada yangu?
Lakini wito huu ulikuwa pia
haukuzaa matunda na hakuna aliyeutilia maanani isipokuwa Ali Ibn Abi Talib
ambaye kwa hali yoyote ile yeye alikuwa ameikubali dini hiyo.
Kwa mujibu wa nyaraka za
kumbukumbu za kihistoria na mashairi yaliyotungwa na Abu Talib ambayo
yanapatikana hadi sasa, Abu Talib pia aliukubali Uislam; hata hivyo, kwa kuwa
alikuwa ndiye mlinzi pekee wa Mtume aliificha imani yake kwa watu ili kuhifadhi
ile nguvu yake ya nje aliyokuwa nayo miongoni mwa watu wa Makkah. Na kuwa
tayari kuitumia nguvu hiyo kumlinda Mtume Muhammad (s.a.w.w) na Uislamu kwa
ujumla. Na alifanya hivyo.
Baada ya kipindi hiki, kwa
mujibu wa maelekezo ya ki-mungu, Mtume akaanza kulingania ujumbe wake kwa uwazi
kabisa. Kwa kuanza kwa kutangazwa kwa wazi kwa ujumbe wake, watu wa Makkah
walikuja juu kwa nguvu sana kwa sababu ya ule ujumbe wenyewe wa uislamu – wa
kuabudu Mungu mmoja na usawa miongoni mwa waumini bila ya kujali tofauti yoyote
ya utaifa, rangi au utajiri – walihofia kabisa dhidi ya hali zao kama
zilivyokuwa. Maumivu makali sana na mateso yalifanywa juu ya Mtume na wale
walioingia kwenye dini hiyo.
Kwa mfano, Bilal, mtumwa wa
kihabeshi ambaye alikuwa ameukubali Uislam, alifungwa kwenye mchanga unaochoma
wa jangwa la Arabia na jiwe kubwa sana likawekwa juu ya kifua chake pamoja na
maonyo kutoka kwa miliki wake Umayya kwamba angeendelea kubakia katika hali
hiyo mpaka atakapoukana Uislam. Lakini sauti pekee ambayo ilisikika ikitoka
kwenye midomo ya Bilal ilikuwa ni “Ahad! Ahad! Ahad!” (Mungu Mmoja! Mungu
Mmoja!
Makuraishi waliwafanyia
waumini ukatili sana kiasi kwamba kikundi cha takriban Waislam 100, chini ya
uongozi wa Ja’far bin Abi Talib waliziacha nyumba zao na mali zao, na wakahamia
Abyssinia (Ethiopia ya sasa).
Nukta Muhimu:
1. waumni
wa mwanzo walikuwa familia ya Mtume (s.a.w.w) sio Abubakar kama wasemavyo
baadhi ya watu.
2. Abu
Talib na familia yake walikuwa ndio waumini wa mwanzo kuuamini Uislamu
3. Uislamu
ni dini ya amani, ndio maana walipoona wanateswa walikimbia badala ya kulipiza
kisasi
4. Uislamu
ulienezwa kwa mawaidha mazuri na mijadala ya kielimu na sio vurugu kama ambavyo
wanafiki na makafiri wanatupakazia.
5. Nasi
tuwe wapenda amani kwetu na nchi zetu zote
Comments
Post a Comment