MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W), KUANZA
KWA UJUMBE
Kwenye umri wa miaka
arobaini, wakati Mtume alipokuwa kwenye faragha ya kiroho ndani ya pango la
Hira, humo alipokea wahyi wa kwanza kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kupitia
kwa Malaika Mkuu Jibril (Gabriel):
Huu ulikuwa ndio mwanzo wa
kazi ya kutangaza dini ya Uislamu. Katika muda huo zile aya tano za mwanzo za
Sura ya 96 ya Qur’an Tukufu zilishushwa kwake. (Tukio hili linajulikana kama
Bi’that – kusimamishwa ili kutangaza ujumbe wa Allah).
Siku ile ile aliueleza Wahyi
huo kwa binamu yake, Ali Ibn Abi Talib ambaye alitangaza kuikubali kwake dini
hiyo.
Baada ya Mtume kurudi
nyumbani na kumueleza mke wake juu ya Wahyi huo, kadhalika na yeye aliukubali
Uislamu. Mara tu, baadaye, Zayd bin Haritha (mtumwa mwaminifu ambaye alimfanya
kama mwanawe mwenyewe) vile vile akasilimu na kuwa naye Muislamu. Hawa ndio
waislamu wa mwanzo kati umma wa Muhammad.
SWALI.
Wale wanaodai kuwa Abubakar
alikuwa wa kwanza kusilimu wana maana gani?
Je Abubakar alikuwa akiishi
kwa Mtume?
Ilikuwaje Abubakar asilimu
kabla ya watu wa nyumbani kwa mtume?
Comments
Post a Comment