JE MASHIA WAMEGAWANYIKA KATIKA
MAKUNDI KAMA WALIVYO MASUNNI?
Mashi’a wamejitoa kwa Allah
(s.w.t.) na ni wafuasi wa Mtume na kizazi chake. Kuna baadhi ya makundi
yamejichukulia jina la Shi’a ili kuwapotosha watu. Wamechukua manufaa ya jina
la Shi’a, wakahubiri imani potofu na kueneza mkanganyiko. Watu wasio na ujuzi
wamehusisha majina yao miongoni mwa Mashi’a. Ziko faraka nne za namna hiyo,
mbili katika hizo zimebakia: Zaidiyya, Kaysaniyya, Qaddahiyya na Ghullat.
Zaidiyya
Zaidiyya wanamfuata Zaid bin Ali
bin Husein. Wanamchukulia mtoto wa Imam Zainu’l- Abidin, aitwaye Zaid kuwa
ndiye Mrithi wake. Kwa wakati huu watu hawa wanapatikana kwa idadi kubwa nchini
Yemen na majirani waizungukao.
Wanaamini kwamba miongoni mwa
Dhuria wa Ali na Fatima, Yeye ndiye “Imam ambaye ni mwanachuo, mcha Mungu, na
shujaa.
Anachomoa upanga na kusimama
dhidi ya maadui,” Katika wakati wa Khalifa dhalimu wa Kibani Umayya, Hisham ibn
Abdul-Malik, Hadhrat Zaid alisimama dhidi ya wale waliokuwa katika mamlaka na
akauawa Shahidi na kwa ajili hiyo akakubaliwa na Zaidiyya kama Imam. Ukweli ni
kwamba Zaid alikuwa ni Sayyid mashuhuri wa ukoo wa Bani Hashim, na alikuwa
akijulikana kwa ucha Mungu wake, hekima, Sala, na ushujaa. Alipitisha mikesha
mingi bila usingizi akikesha kusali na alifunga mara kwa mara. Mtume (s.a.w.w.)
alitabiri Shahada yake (kifo cha kishahidi), kama ilivyosimuliwa na Imam
Husein:
“Mtukufu
Mtume (s.a.w.w.) akaweka mkono wake Mtakatifu kwenye mgongo wangu na akasema:
“Ewe Husein haitachukuwa muda mrefu atazaliwa mtu miongoni mwa Dhuria wako.
Atakuwa anaitwa Zaid; atauwawa
kama Shahid. Katika siku ya ufufuo, yeye na Masahaba zake wataingia Peponi,
wakiweka miguu yao juu ya shingo za watu.” Lakini Zaid mwenyewe hakudai kamwe
kuwa yeye ni Imam. Ni masingizio yasiyo na msingi kwa watu kusema kwamba
alidai. Kusema kweli, yeye alitambua Imam Muhammad Baqir kama Imam na alitoa
utii wake kiukamilifu kwake.
Ilikuwa ni baada tu ya kufariki
kwa Imam Muhammad Baqir ndipo watu wajinga wakatwaa itiqad ya kwamba: “Siye
Imam yule akaaye nyumbani na kujificha machoni mwa watu; Imam ni yule ambaye ni
Dhuria wa Hadharat Fatima, ambaye ni mwenye elimu, na ambaye anachomoa upanga
na kusimama dhidi ya adui, na kulingania (kuwaita) watu upande wake. Zaidiyya
wamegawanyika katika faraka Tano: Mughairiyya; Jarudiyya; Zakariyya;
Khashbiyya; na Khaliqiyya.
Wa-Kaysaniyya Na Imani Yao.
Tapo la pili ni la Kaysaniyya.
Hawa ni Masahaba wa Kaysan, Mtumwa wa Ali bin Abu Talib, ambaye alimuacha huru.
Watu hawa wanaamini kwamba baada ya Imam Hassan na Imam Hussain, Muhammad
Hanafiyya mtoto mwingine (wa kiume) anayefuatia kwa umri, wa Amir’l-Mu’minina,
Ali (A.S.) alikuwa ndiye Imam. Lakini Muhammad Hanafiyya mwenyewe kamwe
hakuwahi kudai hivi.
Alikuwa akiitwa Muaminifu wa
Watiifu. Alikuwa akijulikana sana kwa elimu yake, Ucha Mungu, Utiifu, Ibada, na
mtiifu kwenye maamrisho ya Mwenyezi Mungu. Baadhi ya watu wajinga hutoa
ushahidi ambao waliuita upinzani wake kwa Imam Zainul’l-Abidin. Walidai kwamba
Muhammad Hanafiyya alidai kuwa ni Imam. Ukweli ulikuwa vinginevyo. Hajadai
kamwe kuwa ndiye Imam. Alitaka kuwaonyesha wafuasi wake wajinga cheo na hadhi
ya Imam wa nne, Zainul’l-Abidin. Matokeo yalikuwa kwamba, katika msikiti huohuo
Mtukufu (wa Makka) wakati Hajaru’l-Aswad (jiwe jeusi) lilipothibitisha Uimamu
wa Imam Zainul’l-Abidin, kama ilivyoandikwa kwa mpangilio katika vitabu vya
Ta’rikh, Abu Khalid Kabuli, mkubwa wa wafuasi wa Muhammad Hanafiyya pamoja na wafuasi
wengine, walimkubali Imam Zainu’l-Abidin kama Imam.
Lakini kundi la watu walaghai
walipotosha watu wa kawaida na wajinga kwa kusema kwamba Muhammad Hanafiyya
alionyesha tu adabu, kwamba mbele za Bani Umayya ilikuwa inapendeza mno kwa
Muhammad Hanafiyya kufanya kama alivyofanya.
Baada ya kufariki Muhammad
Hanafiyya, watu hawa walisema hakufa, na kwamba amejificha katika pango la
Mlima Rizwi, na kwamba atakujatokea baadae kuujaza ulimwengu kwa haki na amani.
Tapo hili lina matapo mengine madogodogo: Mukhtariyya; Karbiyya; Ishawiyya na
Harabiyya.
Lakini leo hakuna lililopo hata
moja kati ya hayo.
Qaddahiyya Na Imani Yao.
Tapo la tatu, Gaddahiyya,
Wanajiita wenyewe Shia, lakini ni kundi la Makafiri.
Kitapo hiki kilianzishwa Misri
na Ma’mum Ibn Salim (au Disan) ajulikanae kama Qada na Issa Chahar Lakhtan
(Yesu wa sehemu nne.)
Walijitolea kutafsir Qur’ani
Tukufu na kumbukumbu za Ta’rikh kwa kulingana na matakwa yao. Wanashikilia
kwamba kuna kanuni mbili za dini: moja ya siri na nyingine ya wazi. Kanuni ya
siri ilitolewa na Allah kumpa Mtume Muhammad. Mtume akaitoa kwa Ali, naye
akaitoa kwa dhuria wake na kwa Mashia halisi. Wanaamini kwamba, wale wanaoijua
ile kanuni ya siri wamesamehewa katika Sala na kumuamudu Allah.
Wamesimamisha dini yao katika
nguzo saba. Wanaamini Mitume saba, na Maimamu saba, Imam wa saba akiwa yuko
Ghaibuni. Wanangojea kujitokeza kwake. Wamegawanyika katika vijikundi viwili.
1) Nasiriyya ambao walikuwa
Masahaba wa Nasiri Khusru Alawi, ambaye kwa mashairi yake, hotuba na vitabu
alivuta watu wengi kwenye ukafiri. Walienea katika Tabaristan yote kwa idadi
kubwa.
2) Sabahiyya (wanaojulikana
katika nchi za Magharibi kama ‘Assassins,’ yaani wauaji). Walikuwa ni Masahaba
wa Hasan Sabba, mwenyeji wa Misri ambaye alikwenda Iran, na ambaye alisababisha
matukio ya misiba na huzuni ya Alamut, ambayo ilisababisha kuuwawa kwa idadi
kubwa ya watu. Matapo haya yamehifadhiwa kwenye vitabu vya Ta’rikh.
Ghullat Na Imani Zao
Tapo jingine ni lile la Ghullat,
ambalo ndio kundi potovu zaidi katika matapo yote. Wanajulikana kwa makosa kama
ni Shi’a. Kwa kweli hawa wote ni makafiri. Wamegawanyika katika vijikundi Saba:
Saba’iyya; Mansuriyya; Gharabiyya; Bazishiyya; Yaqubiyya; Isma’iliyya na Azdariyya.
Ghullat wanaitwa Mufawwiza.
Wanaamini kwamba, Allah ameweka au kuaminisha Mamlaka ya mambo yote kwa Maimam
watukufu. Kwa mujibu wao, Maimam ni waumbaji na pia hutupatia sisi riziki. Kwa
uwazi, wale wanaomuona mtu kuwa mshirika katika Mamlaka ya Uungu ni mshirikina.
Sio Shi’a Ithna Shariyya tu
(wanoamini katika Maimam kumi na mbili), bali Waislamu wote ulimwenguni
wanaikataa imani yao.
Shi’a Imamiyya Ithnashariyya Na
Imani Yao.
Hili ndilo kundi Sahihi la
Shi’a, ambalo linaamini Maimamu kumi na mbili baada ya Mtukufu Mtume
(s.a.w.w.). Matapo haya mengine hayana kinachofanana na kundi letu;
wamejichukulia tu jina la Shi’a.
Kwa bahati mbaya watu waovu
huchukua imani za makundi hayo mapotovu na kuunasibisha na Ushia ili tu kupata
sababu za kufitinisha waislamu. Lakini Mashia ni waislamu sahihi na hayo
makundi mengine ndio yaliyopotoka.
Imani Katika Allah Na Mitume
Kundi la Shi’a Imamiyya wanamini
kuwepo kwa Allah Mwenye Enzi zote daima Milele. Ni mmoja, kwa maana kamilifu ya
upweke wa uhalisi wa kuwako kwake. Yeye ni mmoja, hana mfano wake. Yeye ni Muumba
wa vitu vyote vilivyopo. Hakuna chenye kulingana au kuwa sawa na Yeye katika
hali yoyote. Manabii watukufu na Mitume walitumwa kuwaeleza watu kuhusu Allah,
namna ya kumuabudu Yeye, na jinsi ya kumjua Yeye. Mitume wote walihubiri na
kuongoza watu kwa mujibu wa Mafundisho yaliyowekwa mbele na Mitume wakubwa
watano: Nuh, Ibrahim, Musa, Issa na mwisho wa wote, Mtukufu Mtume Muhammad
(s.a.w.w.) ambaye dini yake itabakia mpaka Siku ya Kiyama.
Imani Katika Adhabu, Malipo,
Jahannamu, Pepo, Na Siku Ya Kiyama.
Mwenyezi Mungu Mtukufu ameweka
malipo kwa ajili ya matendo yetu, ambayo yatatole- wa kwetu katika Pepo au
Jahanamu. Siku iliyowekwa kwa malipo ya matendo yetu inaitwa “Siku ya Malipo.”
Wakati maisha ya Ulimwengu huu yatakapokoma, Allah (s.w.t.) atawafufua viumbe
wa ulimwengu kuanzia wa mwanzo mpaka mwisho. Atawafanya wakusanyike katika
Mashar; sehemu ya kukusanyikia Roho zote. Baada ya hesabu ya haki, kila mtu
atapewa malipo au adhabu kwa kulingana na matendo yake.
Mambo haya yametabiriwa katika
vitabu vyote vya Mwenyezi Mungu: Taurat, Zaburi, Injili na Qur’ani Tukufu.
Kwetu sisi Kitabu cha Mwongozo kilicho sahihi zaidi ni Qur’ani Tukufu ambayo
imefika kwetu kutoka wakati wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) bila mabadiliko yoyote.
Tunatenda juu ya amri zilizomo ndani ya Qur’ani Tukufu, na tunataraji malipo
kutoka kwa Allah. Tunaamini katika amri zote zile za wajib ambazo zimo katika
Qur’ani, kama Sala, Saumu, Zaka, Hija na Jihad.
Imani Katika Kanuni Za Ibada:
Halikadhalika, tunaamini katika
Kanuni za utendaji wa ibada, ikiwa ni pamoja na ibada za wajibu na za Sunna na
amri nyingine zote ambazo zimetufikia kupitia kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).
Tumejizatiti kushikamana nazo na kuzitekeleza kwa kadri ya uwezo wetu. Na
tunajiepusha kutokana na madhambi yote, makubwa au madogo kama ulevi, kamari,
uasherati, kulawiti, riba kuua, udhalimu ambavyo vimekatazwa katika Qur’ani
Tukufu na Hadith.
Imani Katika Maimamu:
Sisi Shi’a vilevile tunaamini
kwamba, kama ambavyo kuna mjumbe kutoka kwa Allah ambaye anazifikisha kwetu
sisi kanuni na maamrisho, na ambaye ameteuliwa na kujulishwa kwetu na Allah
(s.w.t.), vilevile kuna mrithi, Khalifa, au Mlinzi wa dini, ambaye anachaguliwa
na Allah na anatambulishwa kwetu kupitia kwa Mtume wa Allah. Kwa ajili hiyo
Mitume wote wa Allah
waliwajulisha warithi wao kwa Umma zao. Wa mwisho wa Mitume watukufu, ambaye
alikuwa ndiye mkamilifu zaidi na aliye nyanyuliwa daraja ya juu zaidi kuliko
Mitume wote wa Allah, aliacha kwa ajili ya wafuasi wake viongozi kusaidia watu
kuepukana na matatizo.
Kwa mujibu wa hadith
zilizothubutu, aliwajulisha kwa watu warithi wake kumi na mbili. Wa kwanza wao
akiwa ni Ali bin Abu Talib (A.s.). Imam wa mwisho, ni Mahdi (A.f) ambaye yupo
ulimwenguni, lakini yuko kwenye Ghaib (amefichwa kwenye macho ya watu),
atatokeza katika muda usiojulikana baadae, wakati atakapoujaza ulimwengu
uliovu- rugika kwa haki na amani.
Shi’a Imamiyya vilevile
Wanaamini kwamba hawa Maimamu kumi na mbili wameteuliwa na Allah na wamejulishwa
kwetu kupitia kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wa mwisho. Wa mwisho katika Maimam
watukufu ametoweka katika macho ya watu (kwa amri ya Mwenyezi Mungu), kama vile
Maimam wengine walivyotoweka katika wakati wa Mitume waliopita, kama
ilivyoelezwa katika vitabu vingi vilivyoandikwa na Maulamaa wenu.
Kiumbe huyu Mtakatifu
amehifadhiwa na Allah (s.w.t.) ili kwamba siku moja aweze kuujaza ulimwengu na
haki. Kwa ufupi, Shi’a wanaamini katika yale yote ambayo yamo katika Qur’ani
Tukufu na katika hadith Sahihi. Ni mwenye kushukuru sana kwa Allah kwamba
nimefuata imani hizi, sio kwa upofu tu wa kufuata wazazi wangu, bali kwa ukweli
wenye mantiki na kuchunguza.
Comments
Post a Comment