KABLA YA UISLAMU, WAARABU WALIKUWA WAUAJI WA WANAWAKE
Mwenyezi Mungu anasema, "Na mmoja katika wao
anapopewa khabari ya mtoto wa kike, husawijika uso wake akajaa sikitiko!.
(Akawa) anajificha na watu kwa sababu ya hatari mbaya aliyoambiwa!
(anafanyashauri) Je, akae naye juu ya fedheha hiyo au amfukie udongoni
(karibuni na hali ya kuwa mzima ili afe)? Sikilizeni! Ni mbaya mno hukumu yao
hiyo. (Qur'ani 16:58-59).
Mara nyingi Mwarabu alimuua mwanae wa kike kwa kuogopa
kwamba angekuwa mateka wa kivita wakati wa vita vya kikabila, na kwa hiyo, kuwa
mtumwa wa adui, na daraja lake kama mtumwa kungeleta aibu kwa familia yake na
kabila lake. Angeweza pia kumuua kwa kuhofia kwake umasikini. Aliamini kwamba
binti yake angekuwa tatizo la kiuchumi kwake. Uislamu ulifanya mauaji ya watoto
kuwa ni dhambi kubwa kabisa.
"Wala msiwaue wana wenu kuogopa umasikini. Sisi tunawaruzuku wao na nyinyi. Hakika kuwaua hao ni hatia kubwa." (Qur'an 17:31).
"Wala msiwaue wana wenu kuogopa umasikini. Sisi tunawaruzuku wao na nyinyi. Hakika kuwaua hao ni hatia kubwa." (Qur'an 17:31).
Vilevile walikuwepo Waarabu ambao hawakuwaua watoto
wao, lakini waliwanyang'anya haki zao zote. Walifikiri kwamba kwa vile binti
zao watakapoolewa watakwenda kuingia nyumba nyingine za waume wao, hapakuwepo
na haja ya kutumia gharama yoyote juu yao. Ilikuwa katika mazingira ya namna
hii ambayo Khadija alizaliwa, akakua na kuishi mazingira ya "kumkataa
mwanamke." Kutokea nyumbani kwake Makka, Khadija aliendesha biashara
iliyokuwa inaendelea kukua na kuenea kwenye nchi za jirani. Kile ambacho
alikwisha faulu kukipata kingekuwa cha kusifika katika nchi yoyote, katika
kipindi chochote na kwa mtu yoyote mwanamume au mwanamke. Lakini mafanikio yake
yamesifika mara mbili pale ambapo mtu atafikiria ule "mfumo-dume" wa
kumpinga mwanamke, ulioendekezwa na Waarabu.
Comments
Post a Comment