KUFUNGWA MILANGO YA NYUMBA ZA MASAHABA

KUFUNGWA MILANGO YA NYUMBA ZA MASAHABA

An-Nasai ametoa katika kitabu chake Kitab al-Khasais fi fadhil Ali ibn Abi Talib ((inaojulikana kwa jina Khasais Nasai) iliopokewa na Zaidi Ibn Arqam kwamba milango ya baadhi ya nyumba za Masahaba  ilifunguka ndani ya msikiti (Masjid-un-Nabi). Kwa maana kuwa wakipitia msikitini kila wanapotaka kutoka nyumbani kwao.

Mtume alitoa amri milango yote ifungwe isipokuwa mlango wa nyumba ya Ali.

Masahaba wakaonyesha uchungu na kutoridhika kwa amri hiyo. Ndipo Mtume akasimama na akawahutubia. Baada ya kumsifu Mola akasema, “Kwa mujibu wa amri ya Mwenyezi Mungu nilikuamrisheni kuifunga milango yenu na Ali aiweke wazi; hoja na mabishano yenu hayatakiwi. Sikufunga wala sikufungua mlango wa mtu yeyote kwa hiyari yangu, bali nilifuata kama nilivyo amrishwa na Mwenyezi Mungu.”

Maswali:
1.  Unajifunza nini katika tukio hili?

2.  Je suala hili halionyeshe ubora wa Imam Ally juu ya Masahaba wengine?

Comments