KUJENGWA KWA MSIKITI WA QUBA

 KUJENGWA KWA MSIKITI WA QUBA

Sheikh Zayn al-Din Umar Ibn al-Wardi katika kitabu chake  Tatimmat al-Mukhtasar fi Akhbar al-Bashar (inayojulikana kwa jina Tarikh Ibn al-Wardi) anaandika kwamba baada ya kufika Mtume Quba akatia msingi wa msikiti wa Quba ambao Mwenyezi Mungu  katika Qur’ani kaitaja hivi “La-Masjidun Ussisa Alat-Taqwa”  (Msikiti uliojengwa juu ya msingi wa kumcha mwenyezi Mungu) (Sura at-Tawba Aya 108).

Na Sheikh Abdul Haq mwanachuoni wa Delhi mpokeaji hadithi anasema katika kitabu chake Jadhbul Quloob  kwamba watu wa Quba walimwomba mtume awajengee msikiti,  basi hapo Mtume “akawataka Masahaba watukufu mmoja wao  ampande ngamia wa Mtume na azunguuke naye.” Mara Abu Bakar akainuka na akampanda huyo ngamia lakini ngamia hata kidogo  hakutikisika wala hakuondoka. Baadaye Umar akajaribu kumpanda na mnyama asiondoke wala kutikisika. Ndipo imam Ali akasimama na kwenda  kumpanda mara alipotia miguu yake katika kikuku cha kupandia tu mara ngamia akanyanyuka. Mtume tena akasema, “Acha hatamu, kwani ameamrishwa na Mwenyezi Mungu azunguke.” Kwa hivyo akachimba msingi wa msikiti kufuatia nyayo (alama) za ngamia, na akawataka watu wa Quba wakusanye mawe. Tena akafanya alama kwa mkuki wake kuonyesha Qibla na akaweka jiwe la msingi kwa mkono wake mtukufu.

MASWALI:
1.  Je kwa nini ngamia hakutembea pale alipopandwa na Abubakar na Umar?
2.  Lakini kwa nini ngamia huyo alikubali kusimama na kuzunguka alipopandwa na Imam Ally?


Bila shaka ngamia alikataa kuzunguka kwa kupandwa na watu hao kwa sababu Allah alitaka kuzuia madhara yao ya baadaye pale ambapo wangeitumia hoja hiyo kuhalisha utawala wao haramu. Kwa madai kuwa wao ndio viongozi sahihi. Hivyo alimngoja khalifa sahihi ndiye amsaidie Mtume katika jukumu la kuweka mipaka ya msikiti huo mtukufu. 

Comments