KUUNGWA UDUGU BAINA YA MUHAJIRINA NA ANSWAR

KUUNGWA UDUGU BAINA YA MUHAJIRINA NA ANSWAR

Abul Fida ameandika, “Basi Mtume (s.a.w.w) katika Madina akaanzisha udugu kati ya Masaba Muhajirina (wahamiaji kutoka Makka) na Ansar  (wasaidizi, watu wa Madina) na akamtukuza Ali kwa udugu pamoja naye. Abu Bakar akafanywa ndugu wa Khaarijah bin Zaid. Kadhalika Abu Ubaydah bin al-Jarrah akafunganishwa udugu na Sa’ad bin Ma’az, na Umar bin Khattab pamoja na Utban bin Malik, Abul-Rahman bin Auf pamoja na Saad bin Rabee, Uthman bin Affan pamoja na Aus bin Thabit, Talha bin Ubaydullah pamoja na Kaab bin Malik na Saeed bin Zaid pamoja na Ubai bin Kaab. Lakini akamtangaza Imam Ally kuwa ni ndugu wa yeye mwenyewe Mtume wa Mwenyezi Mungu.

Sayyid Nuruddin Abul Hasan Ali bin Abdullah al-Samhudi al- Madani ash-Shafii anaandika katika Khulasa al-Wafa kwamba  Mtume (s.a.w.w.) alifanyisha udugu kati ya Muhajirin na Ansar na  aliwaamuru kama kila wawili wawili (mmoja Muhajiri na wa pili  Ansar) waanzishe udugu kati yao; kisha Mtume akashika mkono wa Ali bin Abi Talib na akasema, “Huyu hapa ni ndugu yangu.”

Na Ibn Abdul Bir katika Isteeab, kitabu mashuhuri chenye majina ya Maswahaba wa Mtume, anasema, “Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)  alivyowafanya udugu kati ya muhajirina (wafuasi wake wa Makka)  katika Makka vivi hivi alianzisha kati ya Muhajireen na Ansar katika Madina, na katika matukio yote mawili alimtukuza Ali kwa kumfanya ndugu yake na akasema, ‘Wewe ndugu yangu hapa duniani na vile vile baadaye Akhera.’”

MASWALI:
1.  Je Imam Ally ni Muhajirin au Answar?
2.  Je Mtume ni Muhajirin au Answar?
3.  Kama udugu ulikuwa ufanywe kati ya Muhajirina na Answar, kwa nini Mtume akamtangaza Muhajirin mwenziwe (Imam Ally) kuwa ndugu yake?

4.  Kwa nini asimtangaze Abubakar, kama wanavyodai washabiki wake kuwa yeye ndiye aliyekuwa kipenzi wa Mtume?

Comments