NINI ITIKADI YA MASHIA JUU YA “TAQIYYAH” (KUTODHIHIRISHA IMANI)?

NINI ITIKADI YA MASHIA JUU YA “TAQIYYAH”  (KUTODHIHIRISHA IMANI)?

Itikadi ya Kishia juu ya ‘Taqiyyah’ inaelezwa katika Qur’ani Tukufu na Mwenyezi Mungu: “Anayemkataa Mwenyezi Mungu baada ya  imani yake, isipokuwa yule aliyelazimishwa hali moyo wake unatulia kwa imani...”  (Qur’ani, 16:106).

Vile vile anasema “Walioamini  wasiwafanye makafiri kuwa wapenzi badala  ya wanaoamini, na atakayefanya hivyo, basi  hatakuwa na chochote kwa Mwenyezi  Mungu, ila ya kwamba mjilinde na maovu yao...” (Qur’ani 3:28).

Mwislamu anatakiwa  ayashike maamrisho ya Kiislamu lakini hata hivyo anaweza kwenda kinyume chake (kwa kutodhihirisha) katika wakati wa hatari na mashaka, kama anavyosema Mwenyezi  Mungu: “Mwenyezi Mungu Huwatakieni  yaliyo mepesi wala Hawatakieni yaliyo mazito.” (Qur’ani, 2:78).


Pia Mtume Mtukufu amesema: “Hakuna madhara wala shida katika Uislamu.”

Comments