NINI ITIKADI YA MASHIA JUU YA UKAFIRI NA UISLAMU?

NINI ITIKADI YA MASHIA JUU YA UKAFIRI NA  UISLAMU?

Mashia wanaamini kwamba Mwislamu ni mtu yule ambaye anashuhudia shahada mbili, “Hakuna  Mungu ila Mwenyezi Mungu Mmoja, na  Muhammad ni Mtume Wake.” Isitoshe,  anafuata maamrisho yaliyoletwa na Mtume Mtukufu (s.a.w.) kutoka kwa Mola Wake.

Mtu huyu anastahiki kupewa hifadhi ya nafsi yake, mali na heshima yake na huwa ametakasika. Mambo yanayowahusu Waislamu yanamhusu yeye pia, vile vile mambo yake yanawahusu Waislamu wote.


Kafiri ni yule anayekataa shahada yoyote kati ya hizi mbili, au anakataa jambo lolote  katika mambo ya Kiislamu ambalo linajulikana kuwa ni miongoni mwa mafundisho ya Mtume (s.a.w.).

Comments