CHANZO CHA USHI‘A KUTOKA
VITABU VYA SUNNI
Asili ya Ushi‘a ni sawa sawa na ile ya Uislamu. (Kwa maana
Ushi‘a ndio Uislamu na Uislamu ndio Ushi‘a).
Tofauti kubwa iliyo baina ya Masunni na Mashi‘a ni kuhusu
mshika makamu baada ya Mtume wa Uislamu. Masunni huwamini kwamba Abu Bakar ndiye aliyekuwa mshika makamu wa
kwanza; Mashi‘a huwamini kwamba Ali
ndiye mshika makamu wa haki wa kwanza.
Kama msomi asiye na chuki akichunguza matangazo ya Mtume (s.a.w.w.) kama
yalivyoandikwa na Wanachuoni wa Kisunni katika
tafsir zao za Qur’ani, hadithi za Mtume (s.a.w.w.), wasifu na tarekh
(historia), hana budi kukubali kwamba alikuwa ni Mtume mwenyewe ndiye
muanzilishi wa Ushi‘a.
Tangazo la kwanza la kubaathiwa (Utume wa Muhammad (s.a.w.w.))
limeandamana wakati mmoja na tangazo la ukhalifa la kwanza kutolewa kwa Ali (a.s.).
Tukio hilo linajulikana kama “karamu ya ndugu wa karibu.”
Vifungu vinavyohusu habari hii vimenukuliwa
hapa kutoka kitabu cha Tarikh cha at-Tabari: Ali (a.s.) alisema “wakati
Aya ‘na uwaonye jamaa zako wa karibu’(Qur’ani 26:214), iliposhushwa kwa Mtume wa Allah (s.a.w.w.)
aliniita mimi na akaniamrisha
kutayarisha sa‘ moja (kiasi cha kilo 3) cha chakula na niwakaribishe ukoo
wa Abdu’l Muttalib ili apate kuzungumza
nao. Walikuwa karibu watu arubaini, miongoni mwao walikuwepo ami zake Abu
Talib, Hamza, Abbas na Abu Lahab.
Kisha Mtume wa Allah (s.a.w.w.) akatoa khutba isemayo:- ‘Enyi
watoto wa Abdu’l Muttalib! Simjui mtu yeyote katika bara-Arabu yote ambaye
amewaletea watu wake kitu kilicho bora zaidi kuliko kile nilichokuleteeni mimi.
Nimekuleteeni mema ya hii Dunia na Akhera. Na Allah (s.w.t.) ameniamrisha
nikuiteni ninyi kwake. Ni nani basi
miongoni mwenu atakayenisaidia katika jambo hili, kwa masharti kwamba atakuwa ndugu yangu, wasii wangu na
Khalifa wangu miongoni mwenu?’”
Ali aliendelea kusema: “Hakuna hata mmoja aliyejibu; hivyo
nilisema (ingawa nilikuwa mdogo kuliko wote katika umri): ‘Mimi, ewe Mtume wa
Allah! nitakuwa msaidizi wako katika kazi hii.’ Basi Mtume (s.a.w.w.)
akaweka mkono wake kwenye shingo yangu na kusema: ‘Hakika huyu ni ndugu yangu,
wasii wangu na Khalifa wangu miongoni mwenu. Msikilizeni
na mumtii.’
Waliokuwa kwenye
mkutano wote wakaamka, huku wakicheka na kumuambia Abu Talib kwamba
Muhammad ameamrisha yeye kumsikiliza mtoto wake na kumtii.”
Rejea:
At-Tabari, Muhammad bin Jarir, Tarikh, Juzuu 3 (Laden:
E.J.Brill, 1882- 1885) uk.1171-1173.
Ni kitu cha kushangaza kwamba katika Tarikh ya at-Tabari toleo la Misri (Kairo) 1939 (ambao inadaiwa
kuwa imechekiwa na kile cha toleo la Laden) yale maneno muhimu “wasiyyi wa
Khalifati” (Wasii na Khalifa wangu)
yamebadilishwa kuwa “kadha wa kadha.”
Masikitiko yalioje kuona ulimwengu wa usomi kutoa mhanga uaminifu wake
kwa ajili ya siasa.
Ni lazima itajwe hapa
kwamba hadithi hii pamoja na maneno yake imesimuliwa na wanachuoni wa
Kisunni thelathini, au zaidi, Wanahistoria, Muhaddithina na Mufassirina wa
Qur’ani.
Imam Ahmad bin Hanbal ameisimulia hadithi hii katika Musnad
yake (Juzuu ya 1. uk.111) pamoja na sanad hii ifuatayo (1) Aswad bin Amir
kutoka kwa (2) Sharik, kutoka kwa (3) al-A‘mash kutoka kwa (4) al-Minhal,
kutoka kwa (5) Ibad bin Abdullah al-Asadi, kutoka kwa (6) Ali. Sasa (1), (3) na (5) ni miongoni mwa
wasimuliaji wa hadithi wa al-Bukhari na Muslim, ambapo (2) ni miongoni mwa
wasimuliaji wa hadithi wa Muslim na (4) ni miongoni mwa wale wa al-Bukhari.
Vile vile Ahmad bin Shu’ayb an-Nasa’i ambaye kitabu chake cha
Sunan ni kimoja miongoni mwa vitabu sita
sahihi vya rejea vya hadithi za Masunni, amesimulia hadithi hii kutoka kwa Ibn Abbas katika
kitabu chake al-Khasa’is uk. 6.
Kwa rejea zingine za hadithi hii, tazama al-Muraja’at cha
Abdul Husayn Sharafu d-‘Din (Barua ya 20-23).
Comments
Post a Comment