LENGO LA KUSOMA SIRA
(HISTORIA YA UISLAMU):
Hakika kumfuata Mtume
wa Mwenyezi Mungu na kizazi chake kitakasifu ni kufuata njia iliyonyooka
inayofikisha kwenye wema na ushindi kwa sababu ni njia inayokuepusha na upotovu
na ghadhabu za Mwenyezi Mungu8.
Na ndio njia ya manabii
ambao Mwenyezi Mungu aliwaneemesha kwa neema ya uongofu wake unaowapeleka
kwenye haki. Ndiyo maana akaamrisha kuwafuata, Mwenyezi Mungu akasema: “Hao
ndio ambao Mwenyezi Mungu amewaongoza, basi fuata mwongozo wao.”9
Pia kwa ajili hiyo
ndiyo maana sira ya yule hitimisho la manabii na sira ya mawasii wake
watakasifu imekuwa ni chanzo kati ya vyanzo vya sheria ya kiislamu, na ni
chemchemu ya maarifa na elimu ya kiislamu na ni sawa na Kitabu cha Mwenyezi
Mungu cha milele, kama ilivyoelezea kuhusu hilo Hadithi ya vizito viwili iliyo
mutawatir.
Kama hujaisoma sira ya
viongozi hawa watakatifu itakuwa vigumu huijua na kuifuata. Hivyo kutokusoma
sira ni sawa na kujipoteza njia mwenyewe.
Rejea:
8. Al-Fatiha: 5 – 7.
9. Al-An’aam: 90.
Zaidi ya hapo ni kuwa
sira yao - Amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao wote kwa ujumla - ina faida
kubwa katika kufahamu makusudio ya Kitabu kitakatifu na tafsiri ya Aya zake
tukufu.
Comments
Post a Comment