QUR’AN INASEMAJE KUHUSU
BAADHI YA WAKRISTO
Allah (s.w) anasema kuwa,
“kwa hakika utakuta maadui wakubwa wa waumini ni wayahudi na wapagani, na
utakuta kuwa marafiki wa waumini ni wale wanasema kuwa sisi ni wakristo. Hiyo
ni kwa sababu miongoni mwao kuwa makasisi na watawa. Na wanaposikia ujumbe
ulioteremshwa na Mtume, utawaona wanabubujikwa na machozi kwa kuuona ukweli.
Ndipo watasema, ewe Mungu wetu, tumeamini, kwa hiyo tuweke pamoja na wakweli.
Kwa nini tusimwamini Mwenyezi Mungu na ukweli uliokuja kwetu, ili Mola wetu
atuweke moja na watu wa haki? Kwa hiyo Allah amewalipa kwa hayo wanayoyasema,
pepo (mabustani) inayobubukwa na mito, wakae humo milele. Hayo ndio malipo ya
wafanya mema. 5:82-85”
Kisha Allah anasema, “kisha
tuliwatumia mitume ili wafuate nyayo zao, na tukamtuma Yesu baadaye na tukampa
injil na tukaweka huruma na uvumilivu katika nyoyo za wafuasi wake. Wao
walibuni utawa ambao hatukuwaagiza. Sisi tuliwaagiza kufuata maelekezo ya
Mwenyezi Mungu, lakini hawakulizingatia hili. Hivyo tuliwalipa waaminio
miongoni mwao kwa malipo, lakini wengi wao wamevuka mipaka (57:27).
Japokuwa Allah amewakosoa
wakristo kwa kuvuka mipaka na kuzidisha mambo ambayo hawakuwa wameamrishwa na
yeye, lakini amewasifu vya kutosha kwa kuwa wenye msaada kwa Uislamu na waislamu.
Ukirudi katika historia
utawakuta wakristo waliopambana na kuuawa wakimtetea Mtume Muhammad na familia
yake. Na kwa kufanya hivyo waliutetea Uislamu kwa sababu hawa ndio viongozi wa
Uislamu japokuwa wanafiki na makafiri waliwachukia sana na kuendesha vita dhidi
yao.
Walioendesha vita dhidi ya
Ahlulbayt, mifano yao ni wafuatao, Abubakar bin Quhafa, Umar bin Affan, Yazid
bin Muawiyyah, Aisha bint Abubakar, Twalha, Zuberi, Abdurahman bin Auf, Muawiya
bin Abi Sufian, Yazid bin Muawiya, Hindu mama wa Muawiyah, Abdillah bin Ziyad,
n.k. hawa ndio watu walioendesha operesheni ya kuwatetekeza Ahlulbayt, kila
mmoja alifanya mauaji wakati wa zama zake kwa namna aliyojisikia mwenyewe.
Comments
Post a Comment