USHUHUDA WA JOSHUA
CHARBONNEAU
Joshua Charbonneau ni
muislamu wa Marekani mwenye asili ya Ufaransa. Alizaliwa mwaka 1982 huko
Sumter, South Carolina. Alizaliwa katika familia ya kikristo kisha akasilimu na
kuwa muumini wa Kiislamu afuataye madhehebu ya Shia akiwa na umri wa miaka 17
tu. Hiyo ni baada ya kuzisoma imani, dini na madhehebu yote duniani na kugundua
kuwa dini sahihi ni Uislamu pekee na madhehebu sahihi ni Ushia.
Alipoingia Uislamu alichagua
jina Mateen kwa kiarabu ambalo maana yake kwa kiswahili ni mtu imara na
asiyetetereka. Yeye kama mtaalamu wa kiingereza alijifunza pia kiarabu na
kubobea kabla ya kufikia miaka 26, kisha alihamia Washington DC na kujiunga na
waumini wenziwe katika jiji hilo.
Amewahi kuhojiwa na Al- Anwar
Hussain TV, mahojiano ambayo alipewa kichwa cha habari Safari ya kiroho, ambapo
alieleza namna alivyopambana kutafuta elimu na hatimaye kuuelewa kuwa Ushia
ndio Uislamu sahihih zaidi, na kujiunga nao.
Mwaka 2012 alipata wasaa wa
kusafiri na timu ya television hiyo kutembelea maeneo matakatifu huko Iraq.
Kuanzia mwaka 2013 amekuwa mwanachuo wa hauza chini ya usimamizi wa sheikh
Mustafa Akhound iliyomo katika Imam Ali Center ya Springfield, VA.
Mateen ametengeneza vitabu
kadhaa, kimojawapo kinaitwa Mateso ya Ahlulbayt na wafuasi wao (yaani Mashia)
katika Historia. Kingine kinaitwa wakristo waliopambana na kuuawa kwa kuwalinda
Ahlulbayt wa Mtume Muhammad (s.a.w.w)
Anasema yafuayo kama
utangulizi wa kitabu chake cha wakristo waliopambana na kuuawa wakiwatetea
Ahlulbayt wa Mtume Muhammad (s.a.w.w):
Nilipofanya utafiti katika
historia ya Uislamu niligundua mara nyingi kuwa wakati wa uhai wa Mtume
(s.a.w.w) na pia wakati wa uongozi wa makhalifa 12 watukufu wanatokana na Mtume
mwenyewe (Ahlulbayt), wakristo kadhaa walisimama kupambana dhidi ya dhulma
walizokuwa wakifanyiwa Ahlulbayt wa Mtume.
Nimeshangazwa sana, kwa nini
wakristo hawa walitoa maisha yao kumtetea Mtume na kizazi chake wakati wao
wakiwa waumini wa dini nyingine.
Bila shaka hii imetokana na
tabia za viongozi hawa ambazo zilikuwa takatifu kiasi kwamba hata waabudu
masanamu, wakristo na wayahudi ambao walimchukia sana, lakini wasingeweza
kupata kasoro yoyote ya kuweza kumlaumu Mtume na Ahlulbayt wake.
Hata kabla hajaanza
kuutangaza Uislamu, Mtume aliitwa na makafiri kuwa ni Al-Ameen (mwaminifu) na
Assadiq (mkweli). Watu hawa watukufu walichomoza mwanga wao kwa kila mtu
waliyekutana nao. Tabia zao ziliwafurahisha watu na kuwashuhudisha maadili ya
hali ya juu kiasi kwamba alimhudumia kila mtu kwa haki bila kujali dini yake,
kabila, jinsia wala rangi yake.
Wakristo walikuwa na amani
sana katika serikali ya kiislamu chini ya Uislamu wa kweli wakati wa kipindi
cha Uongozi wa Mtume mwenyewe na pia kipindi kifupi cha uongozi wa Imam Ally
(a.s). kipindi hiki hakuna mkristo aliyedhulumiwa kwa sababu ya dini yake.
Mtume na Ahlulbayt wake
waliamini kuwa ni jukumu lao kuwasaidia watu wote kupata haki zao kwa sababu,
hata kama sio waislamu bado ni wanadamu sawa na waislamu. Hivyo wanamahitaji
sawa na waislamu.
Watawala (makhalifa)
walinyakua madaraka baada ya kifo cha Mtume waliwatesa na kuwaua Ahlulbayt na
Mashia wao kwa wingi. Tendo hili liliwaudhi sana wakristo kiasi kwamba baadhi
yao walijitolea muhanga kuwatetea watukufu hawa.
Nitaandika orodha ya matukio
ya kihistoria yanayoonyesha jinsi Mtume na Ahlulbayt wake walivyowatendea vyema
wakristo katika zama zao. Lakini pia nitaonyesha matukio ambapo wakristo
walisimama kuwatetea Ahlulbayt na wafuasi wake kutokana na dhulma za wanafiki
miongoni mwa wanaojiita waislamu.
Ninapoongelea Uislamu wa
kweli ninakusudia Uislamu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) na Ahlulbayt wake na wala
siongelei Uislamu wa uongo yaani ule unaotokana na watawala waliopora madaraka
na kujipa vyeo vya ukhalifa na kuwatendea waislamu na wasiokuwa waislamu
madhila mengi kwa madai ya kuulinda na kuusambaza Uislamu.
Maswali:
1. Kama Mtume na Ahlulbayt wake waliwatendea wema
makafiri kiasi cha kwamba makafiri waliamini kuwa Mtume ni kiongozi wao na
hivyo kusimama kumtetea yeye na Ahlulbayt wake, je hawa wanaowadhalilisha na
kuwachinja wanadamu (bila kujali dini zao) kwa maelfu ni wafuasi wa nani?
2. Je nasi tunaweza kuishi vyema na watu wa imani
nyingine kama alivyofanya Mtume?
3. Hawa viongozi bandia waliopora madaraka, wanaotajwa
katika habari hii ni akina nani? Wataje.
Comments
Post a Comment