ASILI YA UISLAMU

ASILI YA UISLAMU
Uislamu ni dini ya kimaumbile ya mwanadamu iliyoandaliwa na Muumba ili dini hii tukufu iwaongoze wanadamu wote. Msingi wake mkuu ni tawhid yaani Umoja wa Mungu.

Katika Uislamu watu wanatakiwa kuchagua aidha wafuata muongozo wa Uislamu (Qur’an) au waende kinyume chake. Ukiufuata muongozo Allah atakulipa kheri na ukiupinga muongozo Allah atakuadhibu kwa kukuingiza Jahanam.

Mwenyezi Mungu aliueneza Mfumo huu kupitia mitume wake. Mtume wake wa kwanza alikuwa nabii Adam na Mtume wake wa mwisho ni Mtume Muhammad (s.a.w.w).

Allah alituma mitume wengi kuongoza watu kutokana na tabia mbaya waliyonayo wanadamu, pindi tu Mtume anapoondoka au kufariki dunia, wafuasi wake hurtadi dini na kufuata mifumo batili ya maisha. Mfano ni pale Nabii Mussa alipokwenda mlimani kupokea amri za Allah kwa siku thalathini tu, aliwakuta masahaba wake wamekwisha tengeneza sanamu na kuliabudu.

Kipindi cha uhai wa Mtume Muhammad (s.aw.w), Uislamu ulikuwa mfumo wa mawazo ya aina moja tu. Mara tu alipofariki, ufa wa kwanza ulijitokeza katika ile “nguzo imara” ya Uislamu. Wafuasi wake – Waislamu – walikingamizwa kwenye makundi mawili. Katika kingamizo hili, wengi wa maswahaba zake walikuwa upande mmoja na watu wa nyumbani kwake (Ahlulbayt) kwa upande mwingine. Wakati watu wa nyumbani kwake wakiwa wameshughulishwa na mazishi yake, baadhi ya maswahaba zake walishughulika katika “kuchagua” kiongozi mpya wa kumrithi Mtume.

Katika ule mwanya kati ya kifo na mazishi yake, hili kundi la mwisho (la maswahaba) lilijikusanya katika banda la Saqifah hapo Madina, na likamchagua mmoja (Abubakar) kati yao wenyewe kama mkuu mpya wa umma wa Waislamu. Wao, kisha wakawakabili watu wa ile familia iliyoondokewa kwa jambo lililokwisha fanywa na kuthibitishwa. Mkabiliano huu, kwa bahati mbaya sana, ukawa Sura ya kudumu ya historia ya Waislamu.

Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t,), Rehma na amani juu yake na juu ya Ahlul-Bayt wake, alitokana na ukoo wa Bani Hashim. Baada ya kifo chake mwaka 632 A.D., binamu yake, mkwe wake na mrithi mstahiki wake, Ali ibn Abi Talib, alimfuatia yeye kama mkuu mpya wa Bani Hashim. Wengi wa maswahaba wa Muhammad, Mtume wa Uislamu, walikuwa wamelea uadui wa siri juu yake.

Hawakuweza kumuonyesha uadui wao wakati wa uhai wake Mtume lakini mara walipokuwa na amri juu ya serikali yake hapo Madina, walikuwa wameazimia, kutoiachia, kwa kukosea kwa namna yoyote ile, iangukie kwenye mikono ya Ali ibn Abi Talib.

Watu wa nyumba ya Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) hivyo walizuiwa, kwa nguvu kubwa ya wanadamu, sio tu kwenye urithi wa moja kwa moja bali pia kwenye nafasi zote za mamlaka na madaraka katika serikali za wafuasi wake zilizofuatia.

Marafiki, wafuasi na wanaounga mkono nyumba ya Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.w.t.) wamekuwa kihistoria wakiitwa Shia; na marafiki, wafuasi na wanaowaunga mkono maswahaba, yaani, lile kundi lililofanikiwa kutwaa madaraka hapo Madina, limekuwa likiitwa Sunni. Nitayatofautisha pia makundi haya mawili kwa majina haya.

M. Shibli, mwanahistoria mashuhuri wa Kihindi wa Uislamu, anasema kwamba takriban historia zote za Uislamu zimeandikwa na wanahistoria wa Sunni. Kauli hii inamaanisha kwamba wanazuoni wa Shia hawakuandika historia yoyote ya Uislamu. Kwa nini hawakuandika? Hawakuandika historia kwa sababu ya wazi. Makhalifa wote, masultani na wafalme, wote walikuwa Sunni.

Aliyekuwa Shia hakuruhusiwa kuchapisha ufafanuzi wa historia ya Kiislamu ambao ulikuwa unatofautiana na ule ufafanuzi wa kiserikali, na hakuwa na haja ya kuendeleza kile alichoamini kuwa ni upotoshaji wa ukweli. Yeye, kwa hiyo, aliamua kutoandika historia yoyote kabisa.

Kwa namna hii, yalikuwa ni yale “maelezo” ya kiserikali ya historia ya siku za mwanzo za Uislamu ambayo yalipata kuenea na yakapata kukubalika. Lilikuwa ni jambo la kimantiki kabisa la kufanya kwa serikali za karne za mwanzoni za Uislamu kuingiza kwenye mzunguko, ile hekaya tu, ambayo ilikuwa inakubaliana na itikadi ya kundi lao.

Ilikuwa pia na mantiki kabisa kwa wafuasi wa sera za serikali hizo tunazozizungumzia, kutii itikadi hiyo. Na katika kutii itikadi hiyo ya kundi, kama walihisi kwamba ni muhimu kufunika ukweli, au kwa kiwango chochote, kufunika ule upande mwingine wa Hadith hiyo, ilikuwa na mantiki kabisa kufanya hivyo.

Hakuna jambo lolote la ajabu, la kushangaza au kushitusha katika mwenendo wa wanahistoria wa Sunni. Kitu chenye mantiki kabisa kwao kukifanya kilikuwa, na bado ni, kutetea uhalali wa matukio ambayo yalitukia ndani ya Saqifah, ambamo baadhi ya maswahaba, katika shambulizi la kuwahi kabla ya wengine, walitwaa serikali ya Muhammad, kiongozi wa Arabia.
Kile ambacho hata hivyo ni cha kushangaza na cha kushitusha, ni kwamba wanahistoria wa kimagharibi, yaani, wale Mustashriq, wamemeza, kama jambo la kweli kabisa, kila ambalo wanahistoria wa “baraza” la Kiislamu limewachotea wao kama “ukweli.” Hawa Mustashriq wanadhaniwa kwamba hawana upendeleo, sio wafuasi, na wasiohusika kwa jazba kwa hali yoyote ile. Matokeo ya mashindano fulani katika zama za kale za Uislamu, kwa njia moja au nyingine, yasingeweza kuleta tofauti yoyote kwao.

Na bado, vitabu vya wengi wao vinaonyesha, sio ukweli bali ufafanuzi na propaganda za kundi lililokuwa madarakani. Kwa maana hii, kazi zao ni uigaji wa vile vitabu “vilivyotiwa msukumo” na kile Wakomunisti wanachokiita “jamii inayotawala” ya Waislamu.

Masunni licha ya serikali kuwa chini yao bado hawaridhiki na wala hawatoridhika mpaka wawakandamize na kuwaua wafuasi wa Mtume na Ahlulbayt wake.

Utawasikia wakitoa hadith za uongo kuwa yaliyotokea baina ya masahaba yakaliwe kimya, yaani yasisemwe. Maneno hayo yakwenda kinyume na Qur’an ambayo imesheheni historia za watu na jamii mbalimbali tena ikiwataja kwa uwazi kama walikuwa wema au waovu. Kwa nini masahaba iwe tofauti? Kwa nini tuzuiwe kuwajadili kwa uhalisia? Kama Qur’an imewajadili masahaba wa mitume wengine bila kificho kama ni wema au waovu. Mfano ni ule nilioutoa wa wafuasi wa nabii Mussa. Hapo ongeza wafuasi wa Nuhu na gharika lililowabana.


Hivi watu hawa hawafikiri au ni upofu wa mapenzi? Jiulize Uthuman aliuawa na Masahaba wenzake. Lakini masunni wanasema tusiwajadili na kwamba wote ni wema. Hivi inawezekanaje muuaji na aliyeuawa wote wawe sawa mbele za Allah? Huu ni upofu rohoni. 

Comments