IMAM ALI (AS) NA MFANYA BIASHARA ASIYE NA HESHIMA

IMAM ALI (AS) NA MFANYA BIASHARA ASIYE NA HESHIMA

Imam Ali (as) wakati wa ukhalifa wake, mara nyingi alikuwa akitembelea masoko na kuwashauri na kuwaongoza wafanya biashara.

Siku moja, alipokuwa akipita katika soko la tende, alimuona msichana mdogo akilia, Imam aliuliza sababu ya machozi yake ambapo (msichana) alieleza:

“Bwana wangu alinipa dirham moja (kwa ajili) kununulia tende. Nilizinunua (tende) kwa mfanya biashara huyu, lakini niliporudi nyumbani, bwana wangu alizikataa. Sasa ninataka kuzirudisha lakini mfanya biashara anakataa kuzichua.”

Imam Ali (as) alimgeukia mfanya biashara na kumuambia, “Mtoto huyu ni mtumwa na hana mamlaka yake mwenyewe. Chukua tende na umrudishie fedha yake.”

Mfanya biashara alisogea mbele na huku wafanya biashara na watazamaji wengine wakimtazama, alimpiga Imam kifuani katika jitihada za kumsukuma atoke mbele ya duka lake. Watu waliokuwa wakishuhudia tukio hilo, walikimbia na kumuambia huyo mwanaume:

“Unafikiri unafanya nini? Huyu ni Ali Ibn Abi Talib (as)!”
Uso wa mfanya biashara ulipauka alipokuwa amesimama akaduwaa. Mara moja alichukua tende kutoka kwa msichana na akamkabidhi fedha. Kisha akamgeukia Imam (as) akaomba, “Ewe Amirul Muuminuun! Niwie radhi na nisamehe.”

Imam (as) alijibu,” Nitakuwa radhi na wewe tu pale utakapobadili tabia yako na kuwa njema na ukajali maadili na heshima.”

Mazingatio:
1.    Imam Ally ni kiongozi hata kama mawahhabi na vibaraka wengine wa bani Umaya wanachukia.
2.    Uongozi ni kutumikia watu sio ufisadi wala kuuza sura

3.    Kiongozi anatakiwa ajichanganye na jamii na sio kukaa ikulu pekee na kujifanya mfalme. 

Comments