MAADILI

MAADILI

Allah Mwenye hekima Anasema kumwambia Mtume Muhammad (s.a.w.w):
“Na hakika wewe una tabia tukufu.” (Suratul Qalam: 4).

Mtukufu Mtume (saw) alisema: “Nimetumwa (kama mtume) ili kuja kukamilisha maadili.”
(Jaame Al Saadaat, Juz, 1. Uk. 23)

Uadilifu ni hali ya kuwatendea watu matendo ambayo hata kama ungetendewa wewe ungefurahi. Tena matendo yenye unayafanya bila ubaguzi wala upendeleo.

Kwa mwanadamu, maadili huleta heri na fahari katika ulimwengu huu na wepesi huko Akhera. Kunyanyua hadhi ya mtu katika ukaribu wake kwa Mwenyezi Mungu na humsaidia katika ukamilifu wa dini yake, Mitume wote, mawalii na wateule wa Mwenyezi Mungu walikuwa na maadili ya kupigiwa mfano, na kila mu’umini anapaswa kujipamba kwa maadili hayo, ili mizani ya amali iwe mizito zaidi Siku ya Hukumu.

Mtukufu Mtume (saw) amesema: “Hatima ya muda wetu ni moja, kwa yule mwenye maadili mazuri. Maadili mabaya humfanya mtu ataabike kwa kubanwa mbavu kaburini na (adhabu ya) moto wa jahannam (huko akhera) na ukosefu wa marafiki katika ulimwengu huu.”

Mtu hapaswi kupimwa kwa mujibu wa maarifa yake, utajiri au cheo, bali kwa mujibu wa tabia zenye kusifika, zinazomfanya akubalike mbele ya Allah na kwa kuwa mtukufu na msifiwa mbele ya macho ya watu. (Taz: Tadhkirah al-Haqaaiq, uk. 57)


Ndugu zanguni katika imani tujipe mazoezi ya uadilifu na tuepukane na tabia zote za ukatili, dhulma, uonevu, kujikweza, kujifakharisha, husda, na kila aina ya tabia mbaya. 

Comments