MALIKI ASHTAR, KAMANDA WA MAJESHI YA KIISLAMU

MALIKI ASHTAR, KAMANDA WA MAJESHI YA KIISLAMU

Wakati fulani, Maalik Ashtar alikuwa akipita katika soko la Kufah akionekana masikini sana. Alikuwa amevaa nguo nzito (iliyotengenezwa kwa kitambaa cha turbai) na alikuwa ameweka turbai kichwani kwake badala ya kilemba.

Mmoja wa wafanya biashara alikuwa amekaa dukani mwake macho yake yalipoangukia kwa Maalik. Alimtazama kwa twezo na kwa dharau akamtupia kipande cha udongo.

Maalik alimpuuzia na aliendelea na safari yake. Hata hivyo mtu aliyemtambua Maalik na aliyekuwa ameshuhudia tukio hilo, alimkanya mfanya biashara:

“Aibu juu yako! Unamjua uliyemdhalilisha punde tu?”
“Hapana.” Alijibu mfanya biashara
“Alikuwa ni Maalik Ashtaar, sahaba wa imam Ali (as).”

Baridi iliingia mwilini mwa mfanyabiashara alipowaza juu ya uovu alioufanya. Mara moja aliondoka na kumfuata Maalik ili akaombe msamaha.

Alibaini kwamba Maalik alikuwa ameingia msikitini ambako alikuwa akisali na akamua kumsubiri. Maalik alipomaliza kuswali tu yule mfanya biashara alimuangukia miguuni na kuanza kuibusu, Maalik alimnyanyua na kumuuliza alichokuwa akifanya.

“Ninaomba msamaha kwa dhambi niliyofanya,” alijibu mfanya biashara. Maalik akaeleza, “Hakuna dhambi juu yako. (Naapa) kwa Allah, nilikuja msikitini makhsusi kwa ajili ya kukuombea msamaha.”

Rejea:

Muntahl Aa’maal, Juz. 1, uk. 212; Majumua’h Warraam - Ibn Abi Farraas

Comments