MTUKUFU MTUME (SAW) NA NUA’IMAAN

MTUKUFU MTUME (SAW) NA NUA’IMAAN

Nua’imaan Ibn Amr Ansaari alikuwa ni mmoja wa masahaba wa mwanzo wa Mtukufu Mtume (saw) na alikuwa na maumbile ya uchangamfu na ukarimu.

Imesimuliwa kuwa siku moja Bedui mmoja aliwasili Madina na akampumzisha ngamia wake nyuma ya Msikiti (kisha) akaingia ndani ili awe kwenye hadhara ya Mtukufu Mtume (saw).

Baadhi ya masahaba wa Mtume walimshawishi Nua’imaan kwa kusema “Ikiwa utamuua ngamia huyu, tutagawana nyama yake miongoni mwetu, na Mtukufu Mtume (saw) atalipa bei yake kwa mmiliki.”

Kwa kufuata ushauri wao Nua’imaan alimuua mnyama yule. Mmiliki alipotoka nje ya msikiti na kukuta ngamia wake amekufa alikasirika sana na akaamua kulileta jambo hili mbele ya Mtukufu Mtume (saw). Nua’imaan wakati huo alikuwa amekwishakimbia.

Mtukufu Mtume (saw) alitoka nje ya msikiti, akamuona ngamia aliyekufa na kuuliza “Ni nani anayewajibika kwa kitendo hiki? Wale waliokuwepo walimtuhumu Nua’imaan, hivyo Mtukufu Mtume (saw) akamtuma mtu kwenda kumleta Nua’imaan mbele yake.

Habari zilivuma kuwa Nua’imaan alikuwa amejificha katika nyumba ya Dhubaa’h Bint Zubeir ambayo ilikuwa karibu na msikiti. Alikuwa ameingia kwenye shimo kisha akajifunika na majani mabichi. Mtukufu Mtume (saw) alielezwa juu ya maficho ya Nua’imaan na yeye na masahaba zake wakaelekea kwenye nyumba ya Dhubaa’h walipofika hapo, mjumbe aliomuonyesha Mtume (saw) maficho ya Nua’imaan ambaye Mtume (saw) alimuamuru (mjumbe) alifungue shimo. Baada ya kufanyika hilo, Nua’imaan aliibuka huku mashavu na kipaji chake cha uso vikiwa vimefunikwa na majani mabichi.

Alipomuona, Mtukufu Mtume (saw) alimuuliza “Ewe Nua’imaan! Ni nini hiki ulichokifanya?
Aljibu, “Ewe Mtume wa Allah (Naapa) kwa Allah! hao watu waliokuleta kwenye maficho yangu, ndio hao hao walionishawishi nimuue ngamia!”

Mtukufu Mtume (saw) alitabasamu na kufuta majani kutoka kwenye mashavu na kipaji cha uso cha Nua’imaan kwa mikono yake mitakatifu. Kisha akalipa gharama ya ngamia kwa yule Bedui kwa niaba ya Nua’imaan.

Hapa tunajifunza kuwa:
1.    Tuache unafiki (tuwe wakweli)
2.    Tuache kudanganyana (kupotoshana)

3.    Tuache watu wajifunze ukweli na pia tuwaache waifuate haki 

Comments