UKARIMU
Allah Mwenye Hikma, amesema:
“Kwa hakika Allah yupo
pamoja na wanaojilinda na maovu na wanaofanya wema (kwa wengine).”1
Maelezao mafupi:
Allah humpenda mtu mwenye
sifa ya ukarimu, kama ambavyo tu Allah ameonyesha upole kwetu, ni muhimu kwetu
kuonyesha ukarimu zaidi kwa wengine. Hata kama mtu ametukosea, tunapaswa kujibu
kwa upole na tusilipe uovu kwa uovu, kwani hili litaongeza mafuta kwenye moto
na kuzidisha chuki na uadui.
Mwenendo wa wajumbe(na
Maimamu) wa Allah ulikuwa kwamba wakisalimiwa,
wanaitikia kwa salamu iliyo bora zaidi na kwa ukamilifu zaidi na wakifanyiwa
wema, walikuwa wakiulipa, (tena) kwa kuzidisha (walivyofanyiwa wao).
Wale wanaofanya wema na
kuonyesha ukarimu kwa wengine, huvuta mioyo ya watu, na wakati huohuo matendo
yao yanamuumiza shetani.
Lazima ikumbukwe kwamba wale
wanaofanya wema huwa hawamdhalilishi (wanayemfanyia wema) au kuharibu amali zao
kwa kuweka aina yoyote ya masharti (kwa huyo waliyemfanyia wema).
Myahudi masikini alipata
kukutana na muabudu moto tajiri wakiwa safarini. Muabudu moto aliyekuwa
anamiliki ngamia na masurufu ya kutosha kwa ajili ya safari, alimuuliza, “Ni
nini imani na Itikadi yako?”
Myahudi alijibu, “Ninaamini
kwamba ulimwengu huu una aliyeuumba na ninamuabudu yeye na ninaomba hifadhi
kwake. Ninaonyesha wema kwa yeyote anayeikiri imani yangu, lakini
ninamwaga damu ya yeyote
anayetofautiana na mimi. Ni nini itikadi yako?”
Muabudu moto alijibu, “Nina
wapenda viumbe wote, simdhuru yeyote na ninaonyesha ukarimu na wema kwa
marafiki na maadui pia. Mtu yeyote akinikosea, nina jibu kwa wema kwa sababu
najua kuwa ulimwengu huu una muumba.”
Aliposikia hivi, Myahudi
alisema, “Usidanganye sana. Mimi ni binadamu kama wewe, lakini wakati wewe
unasafiri juu ya ngamia na una masurufu ya safari, hunipi chakula chako wala
huniruhusu nikae kwenye ngamia wako.”
Muabudu moto aliteremka
kutoka kwenye ngamia wake na akatandika kitambaa chini, akaweka chakula chake
mbele ya mwenzake, myahudi alikula mkate na kisha akakaa kwenye ngamia ili
kuondoa uchovu. Walikuwa wamesafari umbali fulani pamoja. Ghafla myahudi
alipompiga ngamia kwa bakora alimlazimisha kukimbia. Yule Mwabudu moto
alimwita:
“Ewe mtu! Nilionyesha upole
kwako lakini sasa, unalipa ukarimu wangu kwa kuniacha peke yangu jangwani!”
Lakini haikujalisha chochote
alichosema, nasaha zake hazikuwa na faida. “Nilikutajia kwamba nina muangamiza
yeyote anaye tofautiana na mimi katika imani na itikadi,” Myahudi alimkemea
huku akikimbia.
Muabudu moto alitazama juu
mbinguni na kuomba: “Ewe Mola wangu! Nimemtendea mtu huyu vyema, lakini
amenilipa uovu. Nitendee uadilifu.”
Alipokuwa akisema haya,
aliendelea na safari yake. Alikuwa amesafiri umbali mfupi tu, ghafla macho yake
yalipoangukia kwenye ngamia wake, aliyekuwa amesimama peke yake baada ya
kumbwaga myahudi chini. Myahudi, aliyekuwa ameumizwa vibaya, alikuwa akilalama
kwa maumivu.
Alikuwa na furaha sana,
muabudu moto alichukua ngamia wake, akapanda mgongoni mwake na alipokuwa
anataka kuondoka Myahudi alilalamika: “Ewe mtu rahimu! Umevuna matunda ya wema
wako na nimeshuhudia matokeo ya uovu wangu; sasa kwa kuzingatia imani zako,
usiondoke katika njia ya wema; kuwa mpole kwangu na usinitelekeze katika jangwa
hili.”
Muabudu moto alijiwa na
huruma na akamruhusu kukaa kwenye ngamia na akampeleka mjini.2
Rejea:
1. Qur’ani Tukufu
Suratu’l-Nahl 16:128
2. Jawaame al–Hikayaat, uk.
24,
Namunah- e ma’arif, Juz. 1, uk. 29
Comments
Post a Comment