KIFO CHA MTUME
NA TUKIO LA SAQIFA
Kwanza; ni
vizuri kujua maana ya neno:
Saqifa: Ni Klabu au ukumbi.
Saqifa: Ni Klabu au ukumbi.
Amesema bibi
Aisha kuwa: "Zilipotangazwa
habari za kifo cha Mtume (s.a.w.) Umar bin Khattab na Mughira bin Shuubam waliingia ndani alikolazwa Mtume (s.a.w.). Umar akasema: Oh msiba mzito kwa kuondokewa na Mtume, kisha
walitoka nje.
habari za kifo cha Mtume (s.a.w.) Umar bin Khattab na Mughira bin Shuubam waliingia ndani alikolazwa Mtume (s.a.w.). Umar akasema: Oh msiba mzito kwa kuondokewa na Mtume, kisha
walitoka nje.
Walipokuwa
mlangoni Mughira akasema: Ewe Umar! Kwa kweli
Mtume amekufa, Umar akajibu: Wewe muongo, Mtume hajafa isipokuwa wewe ni mtu unayesumbuliwa na fitina.Mtume hatakufa mpaka wanafiki wamalizike wote.
Mtume amekufa, Umar akajibu: Wewe muongo, Mtume hajafa isipokuwa wewe ni mtu unayesumbuliwa na fitina.Mtume hatakufa mpaka wanafiki wamalizike wote.
Tazama:
Albidayatu Wannihaya J.5 Uk. 212
Hatimae Umar alikamata
upanga akaonya kuwa: Ye yote atakasesema kuwa Mtume amekufa atakata kichwa
chake.
Alipofika Abubakr,
Umar akanyamaza na akaweka upanga
wake chini. Kisha Abubakr akatangaza kuwa Mtume amekufa, na hapo ndipo alipoondoka yeye na Umar kwenda mwenye ukumbi (Saqifa) wa Bani Saida.
wake chini. Kisha Abubakr akatangaza kuwa Mtume amekufa, na hapo ndipo alipoondoka yeye na Umar kwenda mwenye ukumbi (Saqifa) wa Bani Saida.
Huko walijumuika
na Masahaba kutoka Ansar wa Madina tayari kwa uchaguzi. Abubakr alitoa hutuba
ndefu katika mkutano huo akiwakumbusha kuwa wao (Muhajirina) ndio wenye haki ya
kushika uongozi mahala pa Mtume (s.a.w.).
Hutuba ambayo
ilijibiwa baadaye na Hubab bin Mundhir katika Ansar, naye akionyesha kuwa
ma-Ansar wanayo haki zaidi yao, kwa sababu kwao (Madina) ndiko kuliko shamiri
na kukomaa nguvu za Uislam, na Waislamu kupata Uhuru wa kuabudu. na ikiwa
hapana budi basi kwa Muhajir atoke mmoja na kwa Ansar
atoke mmoja.
atoke mmoja.
Hapo ndipo
Umar aliposimama akasema: "Hilo haliwezekani, panga mbili hazikai katika
ala moja, Wallahi Waarabu hawakubali kuwatawalisheni na hali Mtume wao hatokani
na ninyi".
Baada ya mabishano makali na kushutumiana, karibu wauwane, hatimaye Abubakr akachaguliwa. Kama asemavyo
Umar: "Kuchaguliwa kwa Abubakr kulitokea ghafla, Mwenyezi Mungu alizuia shari zake, na atakayerejesha kitendo kama hiki auliwe".
Tazama:
Tarikhul Tabari J.2 Uk. 446/457
Tarikh Ibn
Athir J.2 Uk. 223
Sahih Bukhar
J.8 Uk. 210
Albidayatu Wannihaya J.5 Uk. 215
Albidayatu Wannihaya J.5 Uk. 215
Abubakr na Umar hawakuwahi kumzika Mtume
(s.a.w.).
Taz: Kanzul Ummal J.5 Uk. 652
Wakati wote huo Imam Ali yuko nyumbani kwa Mtume (s.a.w.)
akishughulikia maandalizi ya kumzika Mtume. Kisha baada ya kumzika Mtume
(s.a.w.) Imam Ali alibaki nyumbani kwake yeye na mkewe Mwana Fatima (a.s.)
wakawa wanakusanyika hapo Bani Hashim.
Abubakr baada ya kutawalishwa alimpeleka Umar bnil Khattab nyumbani kwa Mwana Fatima (a.s.) ili akawatoe wote waende kumbai.
Abubakr akamwagiza kuwa: Endapo watakataa kutoka kuja
kumbai, awauwe. Umar akaenda na kijinga cha moto, Mwana Fatima alipomuona mlangoni na kijinga hicho akamuuliza: Ewe Umar! Umekuja iwasha nyumba yetu? Umar akajibu Ndiyo Wallahi nitakuunguzeni au mtoke kwenda kumbai Abubakr".
kumbai, awauwe. Umar akaenda na kijinga cha moto, Mwana Fatima alipomuona mlangoni na kijinga hicho akamuuliza: Ewe Umar! Umekuja iwasha nyumba yetu? Umar akajibu Ndiyo Wallahi nitakuunguzeni au mtoke kwenda kumbai Abubakr".
Inasemekana kuwa: Umar alipoingia nyumbani kwa Mwana Fatima,
alimpiga ngumi ya tumboni, ngumi ambayo iliumiza ujauzito na kuzaliwa mtoto
aliyekufa! Na kwa sababu ya kipigo hicho, afya ya Mwana Fatima ilidhoofu sana
na baadaye
kufariki baada ya miezi michache tu.
kufariki baada ya miezi michache tu.
Umar alikuwa akiyakumbuka haya, mwenyewe husema "Laiti
ningelikuwa kondoo niliyefugwa, nikanenepeshwa kiasi cha kupendeza. Akija mgeni nikatwekatwe sehemu nyama yangu ikaangwe na sehemu ibanikwe, kisha wanile na wanitoe nikiwa
mavi nisiwe binadamu".
ningelikuwa kondoo niliyefugwa, nikanenepeshwa kiasi cha kupendeza. Akija mgeni nikatwekatwe sehemu nyama yangu ikaangwe na sehemu ibanikwe, kisha wanile na wanitoe nikiwa
mavi nisiwe binadamu".
Taz: Kanzul Ummal J.12 Uk. 619
Comments
Post a Comment