MUUZA DUKA MPUMBAVU

MUUZA DUKA MPUMBAVU

Bwana mmoja mrefu mwenye misuli alikuwa akipita kwenye soko la mji wa Kufa, hatua zake zikuwa imara na za uhakika. Alikuwa na umbo zuri na uso uliobabuka na jua; mapambano kwenye uwanja wa vita yameacha alama kwenye mwili wake na pembeni ya moja ya jicho lake palikuwa na mpasuko.

Mchuuzi mmoja, kwa kuwafurahisha marafiki zake, alimwagia taka mwilini mwake. Yule bwana aliendelea kutembea vile vile bila ya kubadili mwendo wala kumuangalia yule muuza duka. Alipokuwa amekwenda, mmoja wa marafiki wa yule mchuuzi alimuuliza:

“Je huyu bwana uliyemfanyia ufedhuli hivi punde unamjua ni nani?” akajibu, “La simtambui, alikuwa ni mpita njia tu kama wengine wanaopita hapa kila siku. Lakini hebu niambie, ni nani mtu yule?”
“Ajabu! Hamkumjua? Alikuwa ni Malik Ashtar, amiri jeshi mkuu maarufu wa Ali.”

“Ni ajabu kweli! Ashtar huyu huyu ambaye ujasiri wake hugeuza moyo wa simba kuwa maji na ambaye kutajwa kwa jina lake hufanya maadui zake watetemeke kwa hofu?”
“Ndio, yule alikuwa ni Malik Ashtar mwenyewe!”

“Ole wangu! nimefanya nini? Sasa atatoa amri ya kuniadhibu vikali. Ni lazima nimkimbilie sasa hivi nikamtake radhi na kumuomba msamaha kwa adabu yangu mbaya”

Alimkimbilia Malik. Akamuona akigeuka kuelekea msikitini, alimfuata hadi msikitini na kumkuta tayari ameanza kuswali. Alingojea hadi alipomaliza kuswali.

Kwa unyenyekevu kabisa alijitambulisha na akamuambia; “Mimi ndiye yule bwana ambaye ametenda kitendo cha ujinga na kutokuwa na adabu mbele yako”

Malik akamwambia; “Wallahi sikuja msikitini bali ni kwa ajili yako; kwa sababu nilijua kuwa wewe ni mtu jahili na mpotofu na unawapa watu taabu bila ya sababu. Nilikuonea huruma na nimekuja kukuombea na kumuomba Mwenyezi Mungu akuongoze kwenye njia sahihi.


Hapana, kamwe sikuwa na madhumuni kama hayo yaliyokufanya ukawa muoga. Sikukusudia kukuadhibu wala kulipiza kisasi kwa uchafu ulionifanyia. 

Comments