OMBI LA NABII MUSA (AS)

OMBI LA NABII MUSA (AS)

Nabii Musa alipata kumuomba Allah:
“Ewe Mola! Ni utashi wangu kumuona kiumbe wako aliyejitakasa kwa ajili ya ibada Yako na ambaye hajachafuliwa katika utii wake Kwako” Aliambiwa: “Ewe Musa! Nenda katika fukwe za bahari fulani ili nikuonyeshe unachotaka kukiona”

Nabii Musa alikwenda mpaka akafika karibu na bahari. Alipotazama pembeni, aliona kuwa tawi la mti lililokuwa limeinamia juu ya maji, alikuwa amekaa ndege, akiwa amezama katika kumdhikiri Allah.

Musa alipomuuliza ndege (habari zake), ndege alisema: “Tangu Allah aliponiumba, nimekuwa katika tawi hili, nikimuabudu Yeye na dhikiri. Kwa kila dhikiri yangu moja hutokea dhikiri 1000 nyingine, na furaha ninayoipata kutokana na dhikiri ya Allah hunipatia virutubisho.”

“Je unatamani kitu chochote katika ulimwengu huu?”Aliuliza Musa (as). “Ndio. Ninatamani sana kuonja tone moja la maji kutoka kwenye bahari hii.” alijibu ndege. Musa (as) akasema kwa mshangao “Lakini hakuna umbali mkubwa kati ya mdomo wako na maji! Kwa nini hutumbukizi mdomo wako ndani (ya maji) na kunywa?”

Ndege akajibu, “kutokana na hofu kwamba isije ikawa raha inayotokana na maji ikanifanya nisahau raha ya kumdhukuru Mola wangu.” Aliposikia hivi, Nabii Musa (as) alishika kichwa chake kwa mshangao mkubwa.

REJEA:

Khazinah al- Jawaahir, uk. 318

Comments