SHETANI APAMBANA NA
MCHAMUNGU
Katika kabila la Bani
Israil, alipata kuishi mchamungu mmoja. Siku moja watu walimjulisha kuwa katika
sehemu fulani, kulikuwa na mti uliokuwa ukiabudiwa na watu wa kabila hilo.
Aliposikia hivi, aliruka kwa
hasira, akachukuwa shoka yake na kuondoka kwenda kuukata mti ule.
Ibilisi, akatokea mbele yake
kwa sura ya mtu mzee, alimuuliza, “Unakwenda wapi?” alijibu “Nina kusudia
kukata mti ambao unaabudiwa ili badala yake watu wamuabudu Allah.”
“Jizuie mpaka utakaposikia
nitakayoyasema.” Ibilisi alisema kumuambia yule Mchamungu. Yule Mchamungu
akamuambia aendelee kusema. Ibilisi aliendelea: “Allah ana mitume, wake kama
ingekuwa ni muhimu kuuangusha mti angekuwa amewatuma kuja kufanya kazi hiyo.”
Lakini, Mchamungu
hakukubaliana na Ibilisi na akaendelea na safari yake.
“Kwa vyovyote vile
sitakuruhusu” ibilisi alisema kwa hasira na akaanza kupigana mieleka na mtu
yule, katika mpambano huo mchamungu alimbwaga ibilisi chini.
“Subiri nina kitu cha
kukuambia” alisihi ibilisi “Sikiliza! Wewe ni mtu masikini kama ungekuwa na
mali ambayo kwayo ungetoa zaka kwa waumini wengine ingekuwa bora zaidi kuliko
kukata mti. Ukijizuia kukata mti, nitaweka dinari mbili chini ya mto wako kila
siku.”
Mchamungu akasema huku
akiwaza: “Ikiwa unasema ukweli, nitatoa dinari moja kama sadaka na nitaitumia
dinari nyingine.
Hili ni bora kuliko kukata
mti katika hali yoyote, sijatumwa kufanya kazi hii wala mimi sio Mtume mpaka
nijitwishe mzigo wa huzuni na mashaka yasiyo ya lazima.” Hivyo alikubaliana na
ombi la ibilisi na akamuacha.
Kwa siku mbili, alipokea
dinari mbili na akazitumia, lakini katika siku ya tatu, hapakuwa na dalili ya
fedha. Akiwa ameudhika na kusononeka, akachukua shoka yake akatoka kwenda
kukata ule mti.
Njiani alikabiliana na
shetani, aliyemuuliza: “Unaelekea wapi?
“Ninakwenda kukata ule mti.”
“Kwa vyovyote huwezi kwenda
kufanya hivyo” alisema shetani.
Kwa mara nyingine tena
walianza kupambana lakini mara hii ibilisi alimzidi nguvu na akamwangusha
chini, (kisha) akamuamuru, “rudi nyuma sivyo nitatenganisha kichwa na
kiwiliwili chako.”
Mchamungu alisema, “Niache
na nitarudi, lakini niambie ilikuwaje nikaweza kushinda katika tukio la awali?”
Ibilisi alijibu: “Katika
tukio lile umetoka kwa ajili ya Allah na ulikuwa na ikhlasi katika nia yako na
matokeo yake Allah akanidhoofisha kwa ajili yako, lakini safari hii ulikasirika
kwa ajili ya nafsi yako mwenyewe na dinari zako na hivyo nikaweza kukuzidi
nguvu.”
REJEA:
1.
Namunah-e-maarif, Juz. 1, uk. 54;
2.
Ihyaa al- uluum Juz. 4, uk.380;
3.
Riyadh al- Hikaaya, uk.140
Comments
Post a Comment