UNYOFU (UTAKASAJI WA NAFSI)

UNYOFU (UTAKASAJI WA NAFSI)
Allah Mwenye hikma, amesema:
 “Hivyo muabuduni Allah (peke yake) mkiwa waaminifu Kwake katika dini.” (Quran 39:2)

Imam Ali (as) alisema: “Fanya matendo yako kwa unyofu, kwani (ukifanya hivyo) hata kidogo kitakutosha.1

Maelezo mafupi:
Unyofu ni ufunguo wa kukubaliwa amali zote. Mtu ambaye amali zake zimekubaliwa na Allah hata ziwe ndogo kiasi gani, ni mtu mnyofu na mtu ambaye amali zake zimekataliwa na Allah, licha ya wingi wake, sio miongoni mwa watu wanyofu.

Mtu mnyofu hujitahidi kuitakasa roho yake kutokana na maovu na hujibadilisha kufanya amali njema na kudumisha (unyofu wa) nia ili Allah azikubali amali zake.

Kiwango cha nia, maarifa na matendo yanahusiana na utakaso wa kiroho na usafi (wake), na kama mtu mnyofu angezingatia kikamilifu nafsi yake ya ndani, angeitambua dhana halisi ya upweke wa Allah. Kiwango cha chini kabisa cha unyofu ni wakati mtu anapofanya jitihadi kwa kadiri ya uwezo wake wote, akiwa hatarajii malipo kwa matendo yake wala hayapi umuhimu wowote.

Rejea:
1.    Jaame’ al Saadaat Juz. 2, uk. 404 2.

2.    Tadhkirah al Haqaaiq, uk 73

Comments