UZEE NA KUSTAAFU

UZEE NA KUSTAAFU

Mzee mmoja alifanya kazi maisha yake yote; lakini hakuweza kujiwekea akiba ya siku za uzeeni. Na nyakati zake za mwisho alikuja kuwa kipofu pia.

Uzee, umaskini na upofu viliungana mkono, hivyo basi alikuwa hana njia nyingine isipokuwa kuomba. Alikuwa akisimama pembezoni mwa njia kwa ajili ya kuomba. Watu walikuwa wakimwonea huruma na kumpa sadaka ambayo alitumia kwa chakula chake kila siku na hivyo basi aliendelea na maisha yake ya huzuni.

Siku moja imam Ali, Kiongozi wa Waumini alipitia kwenye njia hiyo na kumwona muombaji huyo katika hali hiyo, na kutokana na kujali maslahi ya wengine Ali aliuliza kuhusu huyo mzee. Alikuwa anataka kujua sababu ambazo zilimfanya awe katika hali hiyo. Alikuwa hana mtoto wa kumsaidia? Ama hakuna njia nyingine ya yeye kuishi maisha ya kuheshimika katika uzee wake?”

Watu ambao walimjua mzee huyo walisogea mbele na kumjulisha Ali (a.s.) kuwa alikuwa mkristo na alifanya kazi kwa bidii kwa muda mrefu alipokuwa na macho yake, na ni kijana mwenye nguvu zake. Lakini sasa alivyopoteza ujana wake na pia akawa kipofu hakuweza kufanya kazi yeyote; pia hana chochote alichojiwekea akiba hivyo basi kumlazimu aombe.

Imam Ali (a.s) akasema: “Ajabu! Alipokuwa na nguvu mlifaidika na kazi za nguvu zake, lakini sasa mumemtelekeza peke yake?”
Kisa chake hiki kinaonesha kuwa alifanya kazi alipokuwa na nguvu. Kwa hivyo ni wajibu wa Serikali na Umma kumsaidia hadi atakapofariki. Nendeni mkampe malipo ya maisha ya uzeeni kutoka Hazina ya Taifa.


Hivi ndivyo viongozi wa kiislamu walivyo, humsaidia kila mtu bila kujali dini yake. Ukimwona mtu anajifanya mwislamu halafu kazi yake kuwafanyia fitina watu, hata kama sio wa dini yake basi jua wazi kuwa mtu huyo ni mnafiki, kamwe hawezi kuwa mwislamu wa kweli. 

Comments