KWA NINI KUSOMA MAULIDI?

KWA NINI KUSOMA MAULIDI?

Waislamu husoma maulidi kwa sababu mbalimbali. Kati ya hizo ni:

(i)                 kuikumbuka na kuitukuza siku aliyozaliwa mbora wa viumbe vyote, aliyetutoa vizani na kututia kwenye nuru;

(ii)               ni njia moja ya kutoa shukrani zetu kwa Allah kwa neema hiyo;

(iii)             katika sherehe hizo, hupatikana fursa ya kukumbushana maisha ya bwana mkubwa huyo na mafunzo yake;

(iv)             hupatikana fursa ya Waislamu wa madhihabi na mataifa mbalimbali kushirikiana na kuziweka kando hitilafu zao;

(v)               Mikusanyiko hiyo huleta athari kwa wasio Waislamu ya kuupenda Uislamu, na hata kusilimu.

(vi)             Mikusanyiko hiyo tuambatana na utoaji wa sadaka kwa kutumia pesa na chakula. Hapo watu hupata thawabu zisizo na kifani.


(vii)           Pia mikusanyiko hii huambatana na kumsalia Mtume na ninaamini kuwa kila mtu anajua kuwa Mtume (s.a.w.w) aliwahi kusema kuwa yeyote atakaye mswalia mara moja yeye Mtume atamswalia mara kumi. Hii ni faida kubwa kwa washerekeaji wa maulidi. 

Comments