MIRZA JAWAD AGHA MALIKI
Juu ya mwanazuoni Mirza
Jawad Agha Maliki (aliyekufa mwaka 1343A.H.), imerekodiwa kwamba katika hatua
za awali za kutafuta utakaso wa kiroho na baada ya kuwa amesoma chini ya
mwalimu wake, mwanazuoni mkubwa Mulla Hasainquli Hamadani (aliyekufa mwaka
1311A.H.), kwa miaka miwili mfululizo, alikuwa akilalamika kwa mwalimu wake?
“Katika kutafuta kwangu utakaso wa kiroho, bado sijaweza kupata kitu chochote”.
“Jina lako ni nani?”
aliuliza mwalimu. Akajibu “Wewe hunitambui mimi? Mimi ni Jawad Maliki Tabrizi.”
Hasainquli Hamadani
aliuliza, “Je una uhusiano na familia fulani na familia ya Maliki?” Mirza Jawad
alikubali na kisha akaanza kuzungumza kwa kuwakosoa.
“Wakati wowote utakapofika
wa wewe kuwawekea viatu vyao mbele yao ili wavae, (ambacho unakiona ni kitendo
duni na dhalili), mimi binafsi nitakuja kukuongoza,” alishauri Husainquli
Hamadani.
Siku iliyofuata Mirza Jawad
alipokwenda darasani, alikaa nyuma ya wanafunzi wote na pole pole alianza
kuzoea na kuwa na tabia ya kirafiki na wanafunzi wa familia ya Maliki wanaoishi
Najaf. Iliendelea hivi mpaka ikafikia hatua ambapo alikuwa hata akiwawekea
viatu mbele yao ili wavae.
Ndugu wanaoishi Tibrizi
walipolijua hili, chuki na faraka iliyokuwepo miongoni mwa wanafamilia hao, na
amani ikaanzishwa miongoni mwao.
Baadaye Mirza Jawad
alimwendea mwalimu wake, ambaye alimwambia, “Hakuna maelekezo mapya kwa ajili
yako (Baada ya kuwasuluhisha wana ndugu wa familia ya Maliki). Endelea kufuata
utaratibu huu wa sheria na nufaika kutokana nayo.
Polepole Mirza aliendelea
katika utafutaji wake. Alikuja katika Hauza ya Qum ambapo alianza kuwafundisha
na kuwaongoza wanafunzi katika fani ya utakaso wa kiroho. Idadi kubwa ya watu
wa kawaida na wasomi walinufaika kutokana naye na mafundisho yake.
Huu ndio Uislamu, upendo kwa
wanadamu na kuondoa chuki baina ya watu ili watu waishi kwa amani na upendo.
Comments
Post a Comment