HONGERA RADIO IMAN

HONGERA RADIO IMAN

Assalaam alaykum.

Ninatoa pongezi kwa redio imani kwa kutoa uchambuzi ulio sahihi wa mgogoro wa Mashariki ya kati. Siku za nyuma redio hii ilikuwa ikidai kuwa vita vya mashariki ya kati vinasababishwa na Mashia. Lakini kwa leo, wameweka wazi, uwazi ambao kama watu watakuwa wamewaelewa, vita baina ya waislamu vitapungua kama sio kuisha kabisa. Leo hii wamesema kuwa:

1.    Mashia ni waislamu.
2.    Vita vya mashariki ya kati ni baina ya waislamu kwa maslahi ya makafiri
3.    Vita vya mashariki ya kati ni vya kiuchumi, havina uhusiano na dini yoyote.
4.    Wachochezi wa vita ni nchi za Magharibi na Israel
5.    Ushia na Usunni unatumika na mabeberi ili kutugawa na kututawala tu, si vinginevyo.
6.    Saudi Arabia na washirika wake wametapeliwa kupambana vita vya adui, yaani kumsaidia adui  (mabeberu) dhidi ya adui wao ambaye ni Muiran. Sababu ya wao kutapeliwa ni ujinga.
7.    Waarabu wanatumika na nchi za Magharibi kupambana vita visivyokwisha vya kimadhehebu ili kusahaulishwa mgogoro halisi wa waislam na wayahudi (Au waarabu na wazayuni huko Palestina).
8.    Wafaidika wa vita vya Mashariki ya kati ni waisrael na wamarekani (WAZAYUNI). Waarabu na waajemi ni wahanga wa ubeberu wa wamagharibi.


Baada ya maelezo haya, tutumie akili zetu vizuri, tuwe wamoja, na hivyo kuondoa fikra za migawanyo miongoni mwetu. Hili litavunja njama za maadui za kutuchonganisha.  Hili ni funzo wa sote, sio Mashariki ya kati peke yake. Kwa kutumia uchambuzi huu tupunguza migogo baina ya mashia, baina ya Masunni, baina waislamu na baina na waislam na wasio kuwa waislamu.

Lakini wamefanya kosa moja, kudai kuwa Mashia ni maadui wa wasudia. Hii si kweli kwa sababu sisi wote ni waislamu, hatuwezi kuwa maadui. Qur’an inatuambia kuwa waislamu ni ndugu, ukisema waislamu ni maadui unatupa mashaka kuwa hata sisi sote sio waislamu.

Adui wa Uislamu kwa sasa ni Israel na waitifaki wake. Vita yoyote itakayotangazwa kinyume na hii, ni mchezo wa kibeberu wa kutudhoofisha dhidi ya maadui wetu halisi. Vita hii itawasaidia zaidi maadui kinyume cha fikra za wapenda madhehebu.

Comments