UPOTOSHAJI WA DHANA YA
EVOLUTION
Baadhi ya wanasayansi kwa kupotoshwa au
kutoujua vyema Ukristo walianzisha dhana nyingi kuhusu asili ya dunia na viumbe
vilivyomo.
Nadharia hizi za Kikafiri na Sayansi za Karl Marx pamoja na makafiri wote kwa
ujumla, hudai kuwa nadharia zao ni zao la magunduzi ya kisayansi. Lakini ukizichunguza
nadharia zao si za kisayansi bali ni maelezo ya watu waliochanganyikiwa. Marx
mwenyewe na rafiki yake Engels waliitathmini na kuitumia nadharia ya Darwin ya
“Evolution”.
Marx na Engels
waliiangalia dhana ya chanzo cha mwanaadamu aliyoibuni Darwin kama ni upembuzi
wa kiyakinifu (Dialectical-materialist) katika chanzo chake. Hata hivyo wanasisitiza
kusema kuwa Darwin mwenyewe hakuwa na habari na dhana hiyo (kuwa yeye ni
Mpembuzi - dialectician).
Hivyo basi Marx na
Lenin katika mafundisho yao hawakuegemeza tu katika mafanikio ya elimu ya jamii
na mafunzo ya kihistoria bali pia waliegemeza katika uvumbuzi wa elimu ya
kimaumbile ya wakati wao. Uvumbuzi huu ndio uliokuja kuzaa falsafa ya kisayansi
ijulikanayo kama “dialectical and historical materialism” (uyakinifu wa
kihistoria na kipembuzi).
Lakini je, wagunduzi
wa zama hizo kama Darwin walikuwa wanasayansi kweli? Sayansi ya leo inasemaje
juu ya ugunduzi wao?
Ukafiri si Zao la Sayansi. Yawezekana kabisa kina Darwin walikuwa
wanasayansi wakubwa katika zama zao. Lakini jambo la hakika ni kuwa hawakufahamu kabisa
juu ya uhai na hivyo hawakutumia nadharia za kisayansi katika kuelezea
chanzo cha uhai. Bali walitumia njia iitwayo “Naturalistic point of view”.(Nadharia ya kimaumbile).
Darwin na wenzake
katika moja ya vikao vyao wanakiri kutofahamu uhakika wa uhai katika maeneo
yafuatayo: “The Scientist’s approach to the origin of life is not in
need of an exhaustive definition
of what life is. We must attack from
the naturalistic point of view, namely, that principles unknown or unknowable to
science can not be used to solve
the problem. In other words, we proceed under the assumption that life is a
process that escapes at present our complete
understanding only for reasons of its complexity”.
Tafsiri:
“Mtazamo wa kisayansi juu ya chanzo cha
uhai hauhitaji
kujiuliza uhai (maisha) ni nini. Hatuna
budi kuangalia
nadharia za kimaumbile. Misingi yote
isiyotambulika
kisayansi haiwezi kujibu suala hili. Hivyo
ni lazima tufahamu
kuwa tunaondokea na dhana kuwa uhai
(maisha) uko mbali
na ufahamu wa binaadamu katika maisha ya
leo.”
Maelezo haya ya Darwin
na wenzake yapo wazi – kwamba nadharia zao wamezijenga juu ya dhana tu na
kwamba hawaelewi hakika ya uhai kwa sababu ya utata wake. Bila shaka mwenye
akili timamu hawezi kuikubali nadharia iliyojengwa juu ya dhana na si hivyo tu,
bali dhana ya mtu asiyeelewa hakika ya kitu anachokitolea nadharia.
Jambo la kushangaza
zaidi ni kule kuona jinsi makafiri
wanavyoing’ang’ania
dhana ya Darwin na kuiita ya Kisayansi, wakati Darwin mwenyewe anakiri kuwa
nadharia yake ya ‘evolution’ ni imani tu ambayo hata yeye mwenyewe hawezi
kuithibitisha.
Kwa maneno yake Darwin
anasema: “Lakini naamini mabadiliko ya kimaumbile, sio kwamba naweza kuthibitisha angalau
jamii moja kwamba imebadilika kutoka
hali moja hadi nyingine, ila kwa sababu yanagawanya na kueleza vizuri (kama
nionavyo mimi) ukweli wa mambo juu ya
mgawanyo wa aina mbali mbali, taaluma ya ufanyikaji na ukuaji wa mtoto tumboni
(embryology), ufanyikaji na mgawanyiko
wa miti na wanyama, viungo chipukizi, mabadiliko
ya udongo na mgawanyiko wake.”
Bila shaka maelezo
haya ya Darwin mwenyewe yathibitisha wazi jinsi nadharia ya ‘evolution’
isivyokuwa ya kisayansi. Kwa hivyo basi mtizamo wa makafiri juu ya chanzo cha
uhai na mwanaadamu kwamba hakuna muumba, bali ni zao la “evolution” ni imani
potofu isiyo na misingi ya kisayansi.
Labda ingekuwa vyema
pia kuonyesha hapa kuwa, hata hao
wanasayansi
walioiendeleza dhana ya Darwin ya ‘evolution’ wamekiri kuwa inaudhaifu mkubwa
kwa sababu inashindwa kujibu maswali mengi ya msingi. Bwana Harlay Shapley
katika makala yake “On the Evidences of inorganic evolution”, ana haya ya
kusema:-
“Sababu yetu nzito ni kusema kuwa dunia
nzima iliibuka kama
ilivyo, lakini namna ilivyoibuka, kutoka
wapi na wapi inapoelekea,
ni miongoni mwa masuala tusiyoyajua”.
Nadharia ambayo
inashindwa kujibu maswali hayo ya msingi ni
dhahiri kuwa haiwezi
kutupa jibu sahihi juu ya chanzo cha uhai,
mwanadamu na lengo la
kuumbwa kwake.
Swali la kujiuliza
hapa ni kuwa inakuwaje makafiri kuichukua dhana ambayo udhaifu wake
umeshadhihirishwa si tu na waasisi wake bali hata na dhana yenyewe?
Tumeona kwenye kurasa
za nyuma kuwa Karl Marx alikuwa
miongoni mwa wanafalsafa wa karne ya 19 waliokuwa na
chuki kali dhidi ya Ukristo (dini). Kwa hiyo alikuwa tayari kutumia silaha
yoyote kutokomezea mbali dini. Kinachofanywa na watu hawa ni kuukomoa ukristo
na kwa kufanya hivyo, wanazikomoa dini zote.
Comments
Post a Comment