UTABIRI WA PILI WA MTUME MUHAMMAD NDANI YA BIBLIA
Katika
kumbukumbu la Taurati 33:2-3 imeandikwa hivi, “Bwana
alitoka
Sinai, akawaondokea kutoka Seiri, akaangaza kutoka kilima
cha Parani,
na akaja na elfu kumi za watakatifu. Upande wa mkono
wake wa
kuume palikuwa na sheria ya moto moto kwao. Hakika
awapenda
hayo makabila ya watu, watakatifu wake wote wamo
mkononi
mwako, nao waliketi miguuni pako”.
Hapa
pameelezwa maonyesho matatu ya Mwenyezi Mungu.
1.
Musa alitoka Sinai.
2.
Seiri ni alama ya Yesu.
3.
Na Mtume Muhammad s.a.w. aliangaza kutoka
kilima cha Parani.
Wanazuoni
wamekubali ya kwamba Parani ni kilima cha Makka (Mu’jamul Buldaan).
Biblia inasema.
Ismaili “akakaa katika jangwa la Parani” (Mwanzo 21:21)
na Mtume
Muhammad (s.a.w.w) ni mjukuu wa lsmaili. Huu ni ushahidi kuwa aliyekusudiwa
hapa ni Mtume Muhammad (s.a.w.w).
Mtume s.a.w.
alipoondoka Madina kwenda kuiteka Makka alikuwa na masahaba elfu kumi. Katika
Biblia ya Kiingereza hesabu ya watakatifu hao imetajwa kuwa “ten thousand saints” yaani “watakatifu elfu kumi”,
kama tulivyofasiri hapo juu.
Lakini
katika Biblia ya Kiswahili cha Mvita (Mombasa). Wamefasiri maneno hayo kuwa
“Makumi ya elfu”, yaani elfu zile zilikuwa si kumi moja bali
makumi
mengi, wapate kuwavuruga wasomao Kiswahili wasijue hesabu ya Masahaba
watakatifu wa (Mtume s.a.w.w) aliotokea nao Parani katika utabiri wa Biblia.
lnasikitisha kuona ya kwamba Mapadri na wachungaji hawajatosheka na kiasi hicho
cha uchakachuzi. Katika tafsiri mpya ya Biblia (Union Version) ya mwaka 1952
kifungu hicho cha maneno wamekiandika: “Akaja Meribath kadeshi”, ili wavuruge kabisa
utabiri huyo usiweze kufafanuka. Ni ajabu maneno kama Tirshatha (uk. 478), Darkoni (uk. 479) na mengine yametafsiwa chini
katika kurasa, na mengine yametafsiriwa mwisho wa kitabu cha Biblia, lakini
neno Meribath-kadeshi hawakulieleza chini ya ukurasa ule wala mwisho wa kitabu.
Ingawa ni jipya kabisa lakini
limefanywa
lionekane kama jina la mtu au Malaika au vinginevyo.
Wale wanaofikiri
ya kwamba Biblia ya Union Version imefasiriwa vizuri
sana katika
Kiswahili cha kisasa, watasemaje juu ya uaminifu huu wa wafasiri? llikuwaje
wanazuoni wakubwa wakubwa wa Kiyunani na Kiebrania na Kiswahili kushindwa
kufasiri au kueleza neno Meribath -kadeshi? Inaonekana dhahiri ya kwamba
dhamiri za mapadri zinawalaumu juu ya tafsiri zao zisizo sahihi, zinazovurugwa ili
kuficha haki.
Alama
nyingine ni kuleta Sheria. Mtume Muhammad s.a.w. ndiye aliyeleta Sheria baada
ya Nabii Musa. Na ile Sheria ilileta joto katika mioyo ya Waislamu, nao
wakainuka katika miaka michache. Pia imeitwa “Sheria ya Moto Moto” kwa ajili ya
kuunguza maovu, madhambi na mabaya yote. Wale waliojaribu kuipinga Kurani
wakaangamia wenyewe. Kweli, Kurani ikifuatwa sawa sawa, inaweza kuchoma dhambi
za watu kama moto unavyochoma takataka. Je hamwoni Waarabu waliokuwa wakinywa
ulevi kutwa mara tano waliacha wakawa wanasali kutwa mara tano?
Mtume
alizipenda sana kabila zote. Katika masahaba wake kulikuwa Watu wa makabila
mbali mbali: Waarabu, Wahabeshi, Waajemi na Warumi, na Mtume (s.a.w.w)
aliwapenda wote. Hakuwaita mbwa na nguruwe watu wa mataifa mengine kama
alivyowaita Yesu (Mathayo 7:6; 15:26).
Masahaba wa
Mtume (s.a.w.w) pia walimpenda sana. Kwa hakika Mtume (s.a.w.w) alipendwa na
masahaba zake zaidi kuliko kila mtu anavyopendwa na wafuasi wake. Katika vita,
kama mishale ilipigwa kutoka katika kila upande, masahaba walimzunguka Mtume
kama kuta ili asipate kujeruhiwa. Hatuwezi kuwalinganisha na wanafunzi wa Yesu
waliomtoroka wote wakakimbia na kumwacha Yesu peke yake katika matata (Mathayo
26:56. Marko 14:50).
Ninawakaribisha watu wote katika Uislamu kwa sababu ndio dini sahihi
iliyotabiriwa katika vitabu vilivyotangulia. Kunako majaliwa ya Allah nitaleta
tabiri nyingi zingine kutoka katika vitabu vya kikrito, kiyahudi, kibudha na
hata kihindu.
Comments
Post a Comment