MASHIA WA IMAM ALLY (AS)

Assalaam alaykum;

Asili ya Jina Shia ni Mtume mwenyewe, pale ambapo mara kwa mara alikuwa akiwaashiria wafuasi wa Ali kama Mashi‘a. 

Mwislamu anapokuwa amebobea katika Uislamu wake ndipo hujiongeza na kuwa Mshia. Kwa Lugha nyingine Ushia ni Uislamu ulikokomaa, kama ambavyo uwahhabi au usalafi ukikomaa huwa ugaidi chinjachinja.

Hadithi zifuatazo  zinanukuliwa kutoka rejea za Kisunni:- Ibn ‘Asakir anasimulia kutoka kwa Jabir bin Abdullah kwamba  alisema: “Tulikuwa pamoja na Mtume (s.a.w.w.) wakati Ali alipokuja  (hapo tulipokuwa). Mtume (s.a.w.w.) akasema: ‘Naapa kwa yule  ambaye nafsi yangu ipo mikononi mwake, hakika huyu (Ali) na Shi‘a wake ndio wenye kufuzu siku ya ufufuo.’ 

Kisha Aya ifuatayo ikashushwa.  “Hakika wale walioamini na kutenda mema, basi hao ndio wema wa viumbe. (Qur’ani 98:7)”

At-Tabarani anasema kwamba, Mtume (s.a.w.w.) alimuambia Ali: “Ewe Ali! Hakika utakuja mbele ya Allah, wewe na Shi‘a wako hali ya kuwa mmeridhiwa (na Allah) na hali ya kuwa mnaridhia kwa Allah.”

Kuna hadithi nyingi kutoka kwa wasimuliaji wengi ambazo  wanachuoni wa Kisunni wasingeweza kuzipuuza. Hivyo walijaribu kuzifanya hadithi hizi zioane na upande wao.  Kwa mfano baada ya kunukuu hadithi hizi, Ibn Hajar al-Makki anaandika hivi: “Na Shi‘a wa Ahlul Bayt ni Ahlu’s-Sunnah wa’l-Jamaa (yaani Sunni) kwa sababu ni wao waliowapenda Ahlul Baty kama ilivyoamrishwa na Allah na Mtume wake. Ama wengine, basi wao ni maadui (wa Ahlul bayt).”

Dai hili lilirudiwa tena na Shah Abdu ’l Aziz Dehlawi ambaye  anasema: “Ni lazima ieleweke kwamba Shi‘a wa kwanza (ambao ni Sunni na Tafadhiliyya) katika siku za zamani walijulikana kama Mashi‘a.Wakati Ghulat na Rawafidh, Zaydiyyah na Ismailiyyah  walipochukuwa jina hili kuwa lao...... kwa hivyo wakajichukulia jina  la Ahlu ’s-Sunnah wa’l-Jamaa.”

Ingelikuwa masunni  walikuwa wakiitwa Shi‘a, basi angalau baadhi ya viongozi wa Kisunni  wangelijulikana kwa jina hili kabla ya kuja kwa Zaydiyyah (120 A.H.). Aidha, kama Sunni wangelijulikana kwa jina hili, Zaidiyyah na  Ismailiyyah, wasingeweza kulivumilia jina hili kuwa lao na wangejichagulia jina lingine, haiwezekani mtu achukue jina la adui yake.”

As-Suyuti, Jalalu’d-Din (aliyekufa 910/1504 – 05) katika Tafsiri yake ad-Durrul- Manthur, J. 6 uk. 379. Anasimulia hadithi hii kutoka kwa Ibn Abbas na Ali  kadhalika katika sehemu hiyo hiyo; Al-Khuwarizmi (aliyekufa 569/1173-4) katika al-Manaqib. Hawa wameeleza wazi ubora wa Mashia wa imam Ally mbele za Allah na Mtume wake.

Hadithi nyingine za Mtume (s.a.w.w.) zitamkazo kwamba Shi‘a wa Ali watafuzu siku ya kiyama  zinasimuliwa na Wanachuoni wa Kisunni kutoka kwa Abdullah, Abu Rafi, Jabir bin Abdullah, Ibn Abbas na Ali; Mingoni mwa wanachuoni hawa ni at-Tabarani katika kitabu chake al-Mu‘jam al-Kabir, Ahmad bin Hanbal katika  al-Manaqib yake, Ibn Mardawayh al-Kanji ash-Shafi’i katika kitabu chake Kifayatu ’t-Talib na wengine wengi.

Ibn Athir katika an-Nihayah na Ibn Hajar al-Makki katika as-Sawa‘iqu ’l-Muhriqah (Misri, uk. 92) wanasimulia hadithi nyingi kuhusu suala hili. 

Comments