UTABIRI WA NNE WA MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W) NDANI YA BIBLIA

Kitabu cha Isaya (28:9-13) kinasema, “Atamfundisha nani maarifa?
Atamfahamisha nani habari hii? Je! ni wale walioachishwa maziwa, walioondolewa matitini? Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu ya amri, kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni, huku kidogo na huku kidogo.

La, bali kwa midomo ya watu wageni, na kwa lugha nyingine atasema na watu hawa; ambao aliwaambia, Hii ndiyo raha yenu, mpeni raha yeye aliyechoka; huku ndiko kuburudika; lakini hawakutaka kusikia. “Kwa sababu hiyo neno la Bwana kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo, ili waende na kuanguka nyuma, na kuvunjwa, na kunaswa, na kuchukuliwa”.

Walioachishwa maziwa ni wana wa Ismaili ambao waliakhirishwa kupata ujumbe wa Mungu.

Kur’an tukufu iliteremshwa pole pole, amri juu ya amri, kama ielezavyo bishara hiyo. Baadhi ya sura zilishuka Makka na nyingine Madina (Huku
kidogo na huku kidogo).

Kurani tukufu iliteremshwa katika lugha ya Kiarabu ambayo ni “Midomo ya watu wageni na lugha nyingine” kwa wana wa Israeli.

Awali imeelezwa ya kwamba Mtume (s.a.w.w) atakimbilia Madina kwenye raha, mapumziko na maburudiko, lakini watu wa Makka watazidi kukataa ujumbe wa Uislamu mpaka watashindwa, kuvunjwa na kunaswa, na kuchukuliwa.


Utabiri huu uko wazi sana, atakayebisha ameamua tu kuleta ubishi. Nakuombe acheni ubishi na kujiunga na dini hii takatifu iliyoletwa na mtume huyu wa Mwenyezi Mungu. Nadhani kila mtu anajua kuwa dini ililengwa katika ujumbe huu ni Uislamu peka yake. 

Comments