WAHYI WA PILI KUSHUKA KWA
MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W)
Assalaam alaykum:
Tokea Mtume alipokea wahyi
wa kwanza kwa furaha, kilipita kipindi kifupi tu, Jibril akatokea tena mbele ya
mtume Muhammad (s.a.w.w) wakati alipokuwa ndani ya pango la Hira, na
akawasilisha kwake wahyi wa pili:
“Ewe uliyejifunika (shuka).
Simama na uonye. Na Mola wako mtukuze. (Sura ya 74; Aya ya 1-3).
Hii amri kutoka Mbinguni ya
“simama na uonye” ilikuwa ni ishara kwa mtume kuanza kazi yake.
Jibril alimweleza yeye kazi
zake mpya ya kwanza kabisa ilikuwa ni kuangamiza ibada ya miungu ya uongo, na
kusimamisha beramu ya Tawhid - imani ya Upweke wa Muumba – ulimwenguni; na
alikuwa awaite wanadamu kwenye dini ya Haki – yaani Uislamu.
Uislamu maana yake ni
kunyenyekea kwa Allah (s.w.t.) na kumkubali Muhammad kama mja na Mtume Wake.
Jioni ile mtume alirudi
nyumbani mwenye fahamu na dhamira juu ya kazi yake mpya kwamba alikuwa anapaswa
kuutangaza Uislamu, na kwamba alikuwa aanzie kutoka nyumbani kwake
mwenyewe kwa kuutangaza kwa mkewe.
Mtume alimweleza bi Khadija
juu ya kutembelewa kwa mara ya pili na Jibril, na wajibu uliowekwa juu yake na
Allah (s.w.t.) wa kumwita yeye Khadija kwenye Uislamu. Kwa Khadija, historia na
ukamilifu wa uadilifu wa mume wake vilikuwa ni uthibitisho usiopingika kwamba
alikuwa ni mjumbe wa ki-ungu, na aliukubali Uislamu bila kusita. Kwa kweli,
kati yake na Uislamu, kulikuwa na “uhusiano wa kiitikadi” fulani uliokuwepo
kabla.
Kwa hiyo, wakati Muhammad
Mustafa (s.a.w.w) alipoleta Uislamu kwake, Khadija “aliutambua” mara moja, na
akaufuata kwa matumaini. Aliamini kwamba Muumba ni Mmoja, na kwamba Muhammad
alikuwa ni Mtume Wake, naye akatamka:
“Nashuhudia kwamba hakuna
mungu ila Allah (s.w.t.); na ninashuhudia kwamba Muhammad ni mtumwa na Mtume
Wake.”
Muhammad; huyu Mtume mpya wa
Mungu, alijishindia mfuasi wake wa kwanza - Khadija– mke wake. Alikuwa ndiye wa
kwanza, wa kwanza kabisa kuthibitisha imani yake katika Tawhid (Upweke wa
Muumba), na alikuwa ndiye wa kwanza kabisa kumkubali Muhammad kama Mtume wa
Allah (s.w.t.) kwa wanadamu wote. Alikuwa ndio Mwislamu mwanamke wa kwanza.
Imam Ali Ibn Abi Talib,
alikuwa akiishi wakati huu na walezi wake, mtume Muhammad na Khadija. Wale
vijana wawili wa Muhammad na Khadija – Qasim na Abdullah walikwisha kufa katika
uchanga wao. Baada ya kifo chao, walimchukua Ali kama mtoto wao. Ali alikuwa na
umri wa miaka mitano alipokuja nyumbani kwao, na alikuwa na miaka kumi pale mtume
Muhammad (s.a.w.w) alipotangazwa Mtume wa Allah (s.w.t.) Muhammad na Khadija
walimlea na kumsomesha.
Kwa kuwa imam Ali alikuwa
mmoja wa familia ya Mtume (s.a.w.) mwenyewe, alikuwa bila ya kukwepa, wa kwanza
miongoni mwa wanaume kuupokea ujumbe wa Uislamu. Alishuhudia kwamba Mungu ni
Mmoja, na kwamba Muhammad alikuwa Mtume Wake. Na alikuwa na shauku ya kusimama
nyuma ya mtume kuswali. Kwa vile mtume hakuonekana kamwe kwenye Swala isipokuwa
pale imam Ali alipokuwa pamoja naye.
Mvulana huyu pia alihifadhi
Aya za Qur’an Tukufu kila pale ziliposhushwa kwa mtume. Kwa namna hii, alikua
hasa na Qur’an. Kwa kweli, Ali na Qur’an “vilikuwa” pamoja kama “mapacha” ndani
ya nyumba ya mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w) na Khadija-tul-Kubra (a.s). Mtume
wa Allah (s.w.t.) alikwishapata mwislamu wa kike wa kwanza kwa Khadija, na
mwislamu wa kwanza wa kiume kwa Ali Ibn Abi Talib (a.s).
Comments
Post a Comment