Mwanahistoria Muhammad Ibn
Is’haq Anatuambia:
“Ali alikuwa ndiye mwislamu
wa kwanza kumwamini Mtume wa Allah (s.w.t.) kuswali naye na kuuamini ujumbe
wake mtukufu, alipokuwa ni mvulana wa miaka kumi. Mungu alimpendelea kwa vile
alilelewa katika uangalizi wa Mtume (s.a.w.) kabla Uislamu kuanza rasmi.”(The
life of the Messenger of God).
Mwanahistoria mwingine Muhammad
Husein Haykal Naye Asema:
“Hivyo basi Ali alikuwa ndio
kijana wa kwanza kuingia Uislamu. Alifuatiwa na Zayd ibn Harithah, mtumishi
wake Muhammad. Uislamu ulibakia umefungiwa ndani ya kuta nne za nyumba moja.
mbali na Muhammad mwenyewe, wafuasi wa dini mpya walikuwa ni mkewe, binamu
yake, na mtumishi wake.” (The Life of Muhammad, Cairo, 1935).
Marmaduke Pickhtalls,
anasema:
“Wa mwanzo kati ya wafuasi
wake (Muhammad) alikuwa ni mke wake, Khadija; wa pili binamu yake wa kwanza
Ali, ambaye alimtwaa (kumlea); wa tatu mtumishi wake Zaid, aliyekuwa mtumwa
hapo awali.”(Introduction to the Translation of Holy Qur’an, Lahore, Pakistan,
1975).
Kisha anaendelea, Shahidi wa
tatu kuukubali Uislamu, alikuwa Zayd ibn Harithah, huria wa Muhammad, na mtu wa
nyumba yake.
Tor Andre anatwambia kuwa: “Zayd
alikuwa mmoja wa watu wa mwanzo kuukubali Uislamu, kwa kweli alikuwa wa tatu,
baada ya Khadija na Ali.” (Muhammad, the Man and his Faith, 1960).
Ibn Ishaq anatuhadithia kuwa:
“Kutoka kwa Yahya ibn al-Ash’ath ibn Qays al-Kindi kutoka kwa baba yake, kutoka
kwa babu yake Afiif: anasema Al-Abbas ibn Abdul Muttalib alikuwa rafiki yangu
aliyekuwa akienda mara kwa mara Yemen kununua manukato na kuyauza wakati wa
maonyesho.
Nilikuwa pamoja naye huko
Mina, alikuja mtu katika ujana wa maisha yake na akatekeleza kanuni zote za
wudhu’u na kisha akasimama na kuswali. Kisha akatoka mwanamke akachukua wudhu’u
na akasimama na kuswali. Kisha akatoka kijana anayekaribia utu uzima, akachukua
wudhu’u, kisha akasimama na akasali kando yake.
Nilipomuuliza Al-Abbas ni
nini kilikuwa kinaendelea, akasema kwamba alikuwa ni mpwa wake Muhammad Ibn
Abdullah Ibn Abdul Muttalib, anayedai kwamba Allah (s.w.t.) amemtuma kama
Mtume; yule mwingine ni mtoto wa ndugu yangu, Ali Ibn Abi Talib, ambaye
amemfuata katika dini yake; yule wa tatu ni mke wake, Khadija binti ya
Khuwaylid ambaye pia anamfuata katika dini yake. Afiif alisema baada ya kuwa
amekuwa mwislamu na Uislamu ukiwa umejengeka imara moyoni mwake‘Laiti mimi
ningekuwa wa nne!’ (The Life of the Messenger of God).
Shahidi wa nne aliyeukubali
Uislamu, ni Abu Bakr, mfanya biashara wa Makka.
Hapo mwanzoni, Muhammad
alihubiri Uislamu kwa siri kwa hofu ya kuamsha uhasama wa waabudu masanamu.
Aliwaita tu wale watu kwenye Uislamu ambao alijuana nao yeye binafsi.
Inasemekana kwamba kwa juhudi za Abu Bakr, huyu mwislamu wa nne, watu wengine
wachache wa Makka pia waliukubali Uislamu. Miongoni mwao walikuwa Uthman bin
Affan, Khalifa wa baadae wa Waislamu; Talha, Zubayr, Abdur Rahman bin Auf, Saad
bin Abi Waqqas, na Ubaidullah ibn al-Jarrah.
Kwa muda mrefu Waislamu
walikuwa wachache kwa idadi na hawakuthubutu kuendesha Swala zao hadharani.
Mmoja wa wafuasi wa mwanzo wa Uislamu alikuwa ni Arqam bin Abi al-Arqam, kijana
wa ukoo wa Makhzuum.
Alikuwa tajiri na akiishi
katika nyumba yenye nafasi kubwa katika bonde la Safa. Waislamu walikusanyika
kwenye nyumba yake kuswali Swala zao za jamaa. Miaka mitatu ikapita kwa namna
hii.
Comments
Post a Comment