MFUMO WA JUA (SOLAR SYSTEM)


MFUMO WA JUA (SOLAR SYSTEM)

Kwa mujibu wa taaluma ya sayansi, Dunia (earth) na sayari
nyingine zinazozunguka jua, hufanya ulimwengu (universe) ambao kwa vipimo vyetu vya kibinaadamu ni mkubwa mno.

Dunia (earth) yetu hii ipo umbali wa kiasi cha maili 93 Milioni kutoka kwenye jua. Umbali huu ni mkubwa sana kwa mwanaadamu, lakini ni mdogo sana ukilinganishwa na umbali unaolitenganisha jua na sayari iliyo mbali kuliko zote katika “Solar System” yetu hii, Pluto. Umbali baina ya jua na Pluto ni mara 40 zaidi ya umbali kati ya jua na dunia. Yaani kiasi cha maili 3720 Milioni. Pamoja na kuwa mwanga wa jua husafiri kwa mwendo wa kasi sana – mwendo wa maili 186,000 kwa sekunde, lakini huchukua takriban saa 6 kwa mwanga huo kufikia Pluto.

Dunia ina umbo la duara dufu, yaani duara isiyokamilifu mfano wa chungwa, kwa maana kwamba umbali kutoka ncha ya kaskazini kwenda ncha ya kusini ni mfupi zaidi ya umbali kutoka mashariki mpaka magharibi kwa katikati ya dunia.

Dunia hulizunguka jua katika mzunguko ambao waingereza huuita revolution kwa muda wa mwaka mmoja. Yaani kila mwaka mmoja dunia hukamilisha mzunguko mmoja wa kulizunguka jua. Mzunguko huu ndio huzaa majira mbali mbali ya mwaka, yaani masika na kiangazi kwa uchache.

Dunia pia hujizungusha yenyewe katika mhimili wake. Mzunguko huu waingereza huuita rotation na huichukua dunia siku moja (saa 24) kukamilisha mzunguko wake mmoja wa kujizungusha kwenye mhimili wake. Hatima ya mzunguko huu ni kutengeneza usiku na mchana, kutokana na upande mmoja kuangaziwa na miale ya jua na upande mwingine kuwa gizani.

Huu ndio ulimwengu unaomzunguka mwanadamu kama unavyotambulika na wanasayansi.

Comments