MAPACHA WA ABDI-MANAF NA MAAFA YANAYOTUKUTA WAISLAMU

MAPACHA WA ABDI-MANAF NA MAAFA YANAYOTUKUTA WAISLAMU

Bwana Ibn Athir al-Jazari katika kitabu chake Tarikh al-Kamil anaandika kwamba Abdi-Manaf (Babu wa tatu wa Mtume wetu (s.a.w.w.)) alikuwa na watoto wawili Abdush-Shams na Hashim ambao wazizaliwa mapacha kwa hali kidole cha mmoja wao kiligandana na kipaji cha mwenziwe.
Walipofanyiwa kupasuliwa mahali pale paliposhikamana ikatoka damu nyingi. Wakasema watu: ‘hii ilionyesha kwamba baina ya ukoo wao patamwagika damu nyingi’. Aliposhika Bwana Hashim mahala pa baba yake Abdi-Manaf kuwa yeye mkubwa wa kabila, basi Ummayah mtoto wa Abdush-Shams akaona wivu juu yake, hivyo uadui baina ya watoto wa Hashim na Ummayah ukaanzia hapa.


Katika kitabu cha tafsir mashuhuri kiitwacho Durr al-Mansur cha Jalaluddin Suyuti imeandikwa hivi kwamba Ibn Jaree, Ibn Mundhir, Ibn Abi Hatim, Tabrani, Ibn Mardwaih na Hakim wamehadithia kwa njia sahihi mbali mbali kwamba Ali ameeleza tafsiri ya aya hii: ‘Alam-Tara Ilal-Ladhiyna Bad-Daluu Nia-Matal-Laahi Kufra”. (Je, hukuwaona wale waliobadilisha neema ya Mwenyeezi Mungu kwa kufru) (Sura Ibrahim, Aya 28) hivi, “Wale waliobadili dini ya Mwenyezi Mungu kwa kukufuru ni wana (watoto) wa Umayyah na watoto wa Mugheera, ambao ni wenye kupita kwa dhambi kuliko Quraesh wote.”

Ikumbukwe kuwa katika watoto wa Hashim waliyetajwa hapo awali ndimo alimopatikana Mtume Muhammad (s.a.w.w) na Ahlulbayt wake. Lakini watoto wa Umaya walitajwa kuwa ni waovu kuliko Quraish wote ndimo alimopatikana Uthuman bin Afan, Muawiyyah bin Abi Sufian, Yazid bin Muawiyyah na makhalifa wa uongo wengine waliowatawala waislamu kwa mkono wa chuma huku wakiwaua kwa halaiki kama walivyofanya Yazidi na Baba yake yaani Muawiyyah kwa kuendesha vita dhidi ya Ahlulbayt wa Mtume na kuwaua na kuwanajisi maelfu ya waislamu bila huruma wala chembe ya imani.

Tafadhali tujiepushe kuwafuata viongozi hao halifu kwa sababu mwisho wao haukuwa mwema bila shaka hata wafuasi wao hawatokuwa na mwisho mwema.
Uislamu sahihi ni kumfuata Mtume Muhammad (s.a.w.w) na Ahlulbayt wake.

Comments