MTIZAMO WA KIKAFIRI JUU YA HISTORIA NA UDHAIFU WAKE
Assalaam alaykum.
Historia kwa waandishi wengi wa kileo hufasiriwa kama ni
kumbukumbu ya matendo ya mwanadamu. Matendo hayo yawe ni yenye kumwezesha mwanadamu kupata mahitaji yake muhimu kutoka kwenye maumbile ya asili (nature). Kwa makafiri mahitaji muhimu ya wanadamu ni chakula, nguo na makazi. Kwa hiyo matendo yote ya mwanadamu yana lengo moja tu; la kumpatia mahitaji muhimu ya maisha ambayo ni chakula, nguo na makazi.
kumbukumbu ya matendo ya mwanadamu. Matendo hayo yawe ni yenye kumwezesha mwanadamu kupata mahitaji yake muhimu kutoka kwenye maumbile ya asili (nature). Kwa makafiri mahitaji muhimu ya wanadamu ni chakula, nguo na makazi. Kwa hiyo matendo yote ya mwanadamu yana lengo moja tu; la kumpatia mahitaji muhimu ya maisha ambayo ni chakula, nguo na makazi.
Kwa mtizamo wao huo makafiri wameyahusisha matendo
yote ya mwanadamu na uzalishaji vitu au uzalishaji mali (Material Production). Kwa hiyo basi wakawa wanaiangalia historia katika ngazi mbili. Katika ngazi ya kwanza huiangalia historia kama somo lenye kuelezea mapambano ya mwanadamu dhidi ya mazingira yake. Mapambano ambayo ni ya lazima ili mwanadamu aweze kupiga hatua katika maendeleo.
yote ya mwanadamu na uzalishaji vitu au uzalishaji mali (Material Production). Kwa hiyo basi wakawa wanaiangalia historia katika ngazi mbili. Katika ngazi ya kwanza huiangalia historia kama somo lenye kuelezea mapambano ya mwanadamu dhidi ya mazingira yake. Mapambano ambayo ni ya lazima ili mwanadamu aweze kupiga hatua katika maendeleo.
Katika ngazi ya pili, makafiri huitazama historia kama somo
lenye kuonyesha vipi harakati za uzalishaji mali zinavyoathiri
uhusiano baina ya mtu na mtu.
lenye kuonyesha vipi harakati za uzalishaji mali zinavyoathiri
uhusiano baina ya mtu na mtu.
Hii ni kutokana na imani yao kuwa mwanadamu ni mnyama
kama wanyama wengine. Na badiliko lolote litakalotokea kwa
binadamu aonekane tofauti na wanyama wengine, basi litakuwa ni zao la harakati zake dhidi ya maumbile (Nature). Kwa hiyo kwa makafiri kusoma historia ni muhimu kwa sababu huwasaidia kuelewa mabadiliko ya mahusiano kati ya mtu na mazingira yake na kati ya mtu na mtu. Na kwa njia hiyo wanaweza kufahamu hali ya mwanadamu iliyopita na ya sasa na hivyo kuweza kujiandaa ili kuukabili vyema wakati ujao.
kama wanyama wengine. Na badiliko lolote litakalotokea kwa
binadamu aonekane tofauti na wanyama wengine, basi litakuwa ni zao la harakati zake dhidi ya maumbile (Nature). Kwa hiyo kwa makafiri kusoma historia ni muhimu kwa sababu huwasaidia kuelewa mabadiliko ya mahusiano kati ya mtu na mazingira yake na kati ya mtu na mtu. Na kwa njia hiyo wanaweza kufahamu hali ya mwanadamu iliyopita na ya sasa na hivyo kuweza kujiandaa ili kuukabili vyema wakati ujao.
Mtizamo huu wa makafiri katika kuiainisha historia una udhaifu mkubwa sana. Wao wamemtazama mwanaadamu na mazingira yake au kwa maneno mengine viumbe na mazingira yao na kumwachilia mbali Muumbaji wa vyote hivyo viwili.
Kama wangeingiza kipingele cha Muumba wangefaidika sana kwa sababu lengo la mwanadamu kuumbwa sio kuvaa nguo nzuri au kula sana au kuwa na nyumba nzuri. Bali lengu la kuumbwa mwanadamu ni kumpima na kumwandaa kwa ajili ya maisha ya baadaye huko akhera. Kama ukisahau kujiandaa na akhera ni hasara kubwa sana kwa sababu maisha ya hapa ni mafupi sana na maisha ya akhera ni ya milele. Hivyo utapoteza maisha ya milele kwa sababu ya starehe ya miaka sabini.
Comments
Post a Comment